Afrika: Bara

Afrika ni bara la pili duniani kwa ukubwa, likiwa na eneo la kilometa za mraba zipatazo 30,370,000 na kwa idadi ya wakazi, hao wakiwa 1,225,080,510 (mwaka 2016).

Asia ndiyo bara kubwa pekee zaidi ya Afrika.

Afrika: Jina, Jiografia, Tabianchi
Afrika duniani.
Afrika: Jina, Jiografia, Tabianchi
Afrika kutoka kwenye Mwezi (Ocktoba 2015)
Afrika: Jina, Jiografia, Tabianchi
Uwiano kati ya Afrika, Asia na Amerika.

Jina

Afrika: Jina, Jiografia, Tabianchi 
Afrika kutoka satelaiti.

Neno "Afrika" limetokana na lugha ya Kilatini ya Roma ya Kale. kwa jina hilo Waroma wa Kale walitaja eneo katika Tunisia ya leo, hawakumaanisha bara lote.

Inasemekana asili yake ni kabila la "Afrig" lililoishi sehemu zile,lakini kuna pia maelezo mengine tofautitofauti.

Wakati huo Wagiriki wa Kale walitumia zaidi jina la Libya kwa ajili ya nchi kusini kwa Bahari ya Mediteranea, upande wa magharibi wa Misri.

Maeneo ya ndani kuelekea kusini mara nyingi yaliitwa kwa jina la "Ethiopia" linalomaanisha nchi ya watu weusiweusi (kwa Kigiriki "aithiops": aliyechomwa na jua).

Katika ramani za kale kutoka Ulaya maneno yote matatu ya "Afrika", "Lybia" na "Ethiopia" yanapatikana yakitumika kama jina la bara zima. Jina la "Afrika" limekuwa la kawaida kuanzia karne ya 16 BK.

Jiografia

Afrika imezungukwa na bahari karibu pande zote. Kuna kiungo chembamba cha nchi kavu upande wa kaskazini mashariki na bara la Asia kwenye rasi ya Sinai .

Upande wa kaskazini iko Bahari ya Mediteranea, upande wa mashariki kuna Bahari Hindi pamoja na Bahari ya Shamu na upande wa magharibi iko Bahari Atlantiki.

Kuna kisiwa kikubwa cha Madagaska na funguvisiwa mbalimbali.

Barani kuna nchi huru 54 zinazotambuliwa na Umoja wa Mataifa, maeneo 9 yenye hali ya pekee na madola mawili ambayo yanajitawala bila kutambuliwa kimataifa.

Kuna umbali wa kilomita 8,000 kutoka Ras ben Sakka nchini Tunisia (37°21' N, sehemu ya kaskazini kabisa) hadi rasi ya Cape Agulhas nchini Afrika Kusini (34°51'15" S, sehemu ya kusini kabisa).

Umbali ni km 7,400 kutoka upande wa magharibi (rasi ya Cape Verde, 17°33'22" W) hadi mashariki (Ras Hafun nchini Somalia, 51°27'52" E).

Pwani yote ya Afrika ina urefu wa kilomita 26,000.

Nchi kubwa ya Afrika ni Algeria na nchi ndogo ni funguvisiwa la Shelisheli katika Bahari Hindi. Nchi ndogo Afrika bara ni Gambia.

Kijiolojia Afrika iko kwenye bamba la Afrika. Lile bamba la gandunia la Afrika linaenea mbali zaidi kuliko maeneo tunayotazama kuwa Afrika kijiografia, ni pamoja na maeneo chini ya bahari linapopakana na mabamba ya Ulaya-Asia, Uarabuni, Uhindi na Australia, Antaktika, Amerika ya Kusini na Kaskazini. Upande wa mashariki wa bamba la Afrika kuna ufa unaozidi kupanuka ikielekea kujitenga kutoka Afrika kama bamba la Somalia.

Tabianchi

Afrika: Jina, Jiografia, Tabianchi 
Uoto barani Afrika

Tabianchi[dead link] ya Afrika ni pana, kuanzia kanda za tropiki hadi kufikia maeneo ya nusu-aktiki (baridi) kwenye ncha za milima mirefu.

Nusu ya kaskazini ya bara ni jangwa au angalau yabisi. Sehemu za kati na za kusini zina maeneo ya savanna na kanda za msitu wa mvua.

Afrika ni bara lenye joto kuliko mabara yote na asilimia 60 za uso wake ni maeneo yabisi au jangwa.

Nchi za Afrika


Wakazi

Afrika: Jina, Jiografia, Tabianchi 
Mwanamke wa Benin.

Wataalamu wengi wanakubaliana kutambua Afrika kama asili ya binadamu wote walioko duniani.

Mwaka 2010 idadi ya wakazi wa nchi zote za Afrika ilipita bilioni 1. Ni kwamba idadi yao imeongezeka sana katika miaka 40 iliyopita, ikipiku zile za Ulaya na Amerika.

Ilhali mwaka 1950 walikuwepo Waafrika milioni 229 pekee, idadi iliongezeka kuwa milioni 630 mwaka 1990 na milioni 1200 mnamo 2014.

Hivyo asilimia ya watoto na vijana ni kubwa. Kuna nchi kadhaa ambako zaidi ya nusu ya wananchi wako chini ya umri wa miaka 25. Wakazi wa Afrika ni vijana kuliko wale wa mabara mengine yote; mwaka 2012 umri wa wastani ulikuwa miaka 19.7, wakati kidunia ulikuwa 30.4.

Afrika: Jina, Jiografia, Tabianchi

Lugha

Afrika: Jina, Jiografia, Tabianchi 
Ramani ya lugha za Afrika:      Lugha za Kiafrika-Kiasia      Lugha za Austronesia      Lugha za Kihindi-Kiulaya      Lugha za Khoisan Lugha za Kikongo-Kiniger:      Lugha za Kibantu      Lugha za Kisudani za Kati na Mashariki      Central Bantoid      Eastern Bantoid      Guinean      Lugha za Kimande      Western Bantoid Lugha za Kinilo-Sahara:      Kanuri      Nilotic      Lugha za Kisonghai

Zaidi ya lugha elfu za Kiafrika zinazungumzwa barani leo, ingawa nyingi zinazidi kufifia.

Kusini mwa Afrika, Afrika Mashariki na ya Kati watu wengi ni wasemaji wa lugha za Kibantu (kwa mfano Kiswahili). Asili yao ilikuwa pande za kusini za kanda ya Sahel na kutoka kule walienea katika sehemu nyingi za Afrika upande wa kusini kwa Sahara.

Kuna pia vikundi vya wasemaji wa lugha za Kinilo-Sahara waliofika hadi Afrika ya Mashariki.

Wakazi asilia siku hizi wako wachache, wakionekana kama wasemaji wa lugha za Khoisan au za Wabilikimo.

Watu wa Afrika Magharibi husema zaidi Lugha za Kiniger-Kongo hasa zisizo za Kibantu, pamoja na wasemaji wa lugha za Kinilo-Sahara.

Watu wa Afrika ya Kaskazini kiasili walikuwa hasa wa makundi matatu:

  • Waberber upande wa magharibi
  • Wamisri upande wa mashariki
  • wasemaji wa lugha za Kinilo-Sahara

Waarabu waliovamia eneo hilo lote tangu karne ya 7 BK wameleta lugha yao pamoja na dini ya Uislamu. Lugha yao imekuwa lugha ya watu wengi siku hizi. Wasemaji wa Kiberber bado wako wengi kidogo Moroko na Algeria na wachache katika sehemu za Tunisia na Libya.

Kutokana na ukoloni, lugha za Kihindi-Kiulaya zinazumgumzwa pia, hasa Kiingereza, Kifaransa na Kireno.

Kiafrikaans ni lugha ya pekee ya Afrika Kusini yenye asili ya Ulaya.

Katika kisiwa cha Madagaska kwenye Bahari ya Hindi, inatumika lugha ya Kimalagasy, ambayo ni kati ya lugha za Austronesia.

Dini

Afrika: Jina, Jiografia, Tabianchi 
Ramani ya dini barani Afrika.

Waafrika wana imani za dini nyingi tofauti, lakini takwimu zinazotolewa hazina hakika, pia kwa sababu suala hilo ni nyeti kisiasa kwa serikali zenye mchanganyiko mkubwa wa watu, kama vile Nigeria, Ethiopia na Tanzania.

Kadiri ya World Book Encyclopedia, Islam ndiyo inayoongoza, ikifuatwa na Ukristo. Kumbe kadiri ya Encyclopedia Britannica, 45% za wakazi ni Wakristo, 40% ni Waislamu na 10% wanafuata dini asilia za Kiafrika. Wachache tu ni Wahindu, Wabuddha, Wabaha'i au hawana dini yoyote.

Tazama pia

Tanbihi

Marejeo

Viungo vya nje

    Historia
    Habari

Tags:

Afrika JinaAfrika JiografiaAfrika TabianchiAfrika Nchi za Afrika WakaziAfrika LughaAfrika DiniAfrika Tazama piaAfrika TanbihiAfrika MarejeoAfrika Viungo vya njeAfrika2016AsiaBaraDunianiIdadiKilometa za mraba

🔥 Trending searches on Wiki Kiswahili:

Philip Isdor MpangoJiniKishazi tegemeziDamuMkonoUtamaduni wa KitanzaniaMimba kuharibikaKihusishiVivumishi vya ambaJamhuri ya Watu wa ZanzibarMohamed HusseiniOrodha ya mikoa ya Tanzania na Pato la TaifaMkoa wa TaboraVisakaleKukuYoung Africans S.C.KoroshoVita ya uhuru wa MarekaniLahajaBarua pepeTaswira katika fasihiBonde la Ufa la Afrika ya MasharikiMjasiriamaliMJMeta PlatformsMafumbo (semi)Uzazi wa mpangoMkoa wa ShinyangaMkoa wa MbeyaAlama ya uakifishajiUkongaJipuKassim MajaliwaBurundiMbuTetekuwangaIsimujamiiMaambukizi ya njia za mkojoMwanamkeKiburiVivumishi vya jina kwa jinaKibu DenisBendera ya ZanzibarUnyevuangaUmoja wa AfrikaOmmy DimpozAdolf HitlerAdhuhuriBenki ya DuniaMakabila ya IsraeliEe Mungu Nguvu YetuYesuKibodiOrodha ya visiwa vya TanzaniaBiblia ya KikristoWaziri Mkuu wa TanzaniaTarbiaUhifadhi wa fasihi simuliziTanganyikaSaida KaroliMwanzoIlluminatiWahayaNusuirabuKomaKadi za mialikoVirusi vya CoronaKisimaMaji kujaa na kupwaMeridianiRayvannyHomoniFigoDola la RomaMaradhi ya zinaa🡆 More