Uhifadhi Wa Fasihi Simulizi

Uhifadhi wa fasihi simulizi ni juhudi zinazofanywa kwa makusudi ya kuhakikisha kazi za fasihi simulizi zisisahaulike na hatimaye kupotea kabisa.

Uhifadhi Wa Fasihi Simulizi
Mzee wa Kyrgyzia akisimulia Utendi wa Manas huko Karakol.

Kazi hizo zimeanza tangu binadamu walipoanza kupambana na mazingira yao ya kuishi pamoja. Kazi hizo zilisimuliwa na kuakisi shughuli zilizokuwa zikifanywa na watu katika mazingira ya wakati huo. Kadiri mazingira yalivyobadilika hali kadhalika mambo yaliyokuwa yakisimuliwa ndivyo yalivyokuwa yakibadilika. Hivyo, kulikuwepo na haja ya kuhifadhi kazi hizo kwa faida ya vizazi vipya.

Katika kuhifadhi kazi hizo, kuna njia mbalimbali zilizotumika tangu kale na nyingine zinazotumika leo kwa kufaidika na maendeleo ya teknolojia. Njia hizo ni:

(a) Kichwani / Akilini

(b) Kwa maandishi

(c) Kwa vinasa sauti

(d) Kwa kanda za video, runinga na tarakilishi

(a) Kichwani

Kazi ya fasihi simulizi huwa katika hali ya masimulizi, hivyo mara nyingi huhifadhiwa katika akili ya mtu. Fasihi simulizi ikihifadhiwa kichwani huendelea kuwa hai kwani hadhira na fanani huweza kuwasiliana ana kwa ana. Hadhira huweza kumpongeza au kumhoji fanani papo kwa papo.

Udhaifu wa njia hii

  • Kusahau
  • Kufa kwa fanani au msimuliaji
  • Msimuliaji anaweza kuacha mambo muhimu.

(b) Maandishi

Fasihi simulizi huweza kuhifadhiwa katika maandishi. Mfano kwenye vitabu, vijarida na kadhalika. Fasihi simulizi ikihifadhiwa k2a njia hii haiwezi kupotea wala kubadilika. Njia hii inaweza kutunza kumbukumbu ya kudumu.

Udhaifu wa njia hii

  • Gharama
  • Hubagua (wale wanaojua kusoma tu)
  • Haipokei mabadiliko ya papo kwa papo
  • Baadhi ya vitendo havionekani.

(c) Vinasa sauti

Hizi ni zana zinazotumika katika kurekodi sauti. Mfano wa zana hizo ni tepurekoda au santuri. Katika njia hii, ukweli wa sanaa ya kazi haitabadilika, sauti halisi ya wahusika itaendelea kusikika kama ilivotolewa. Hivyo, fasihi simulizi haipotei wala kubadilikabadilika.

Udhaifu wa njia hii

  • Gharama
  • Kutobadilika kulingana na mazingira na wakati.
  • Utendaji wa wahusika hauonekani.
  • Zana hizo zinaweza kuharibika au kupotea

(d) Kanda za video/Runinga/Tarakilishi

Njia hii huweza kutumika katika kurekodi picha pamoja na sauti kisha kuzionyesha katika runinga au tarakilishi.

Udhaifu wa njia hii

  • Gharama
  • Kutobadilika kulingana na mazingira na wakati.
  • Zana hizo zinaweza kupotea au kuharibika.

Umuhimu wa kuhifadhi kazi za fasihi simulizi

Fasihi simulizi ikihifadhiwa kuna faida mbalimbali zinazojitokeza. Miongoni mwa faida hizo ni:

i) Kutopotea kwa kazi hizo: Fasihi simulizi ikihifadhiwa uwezekano wa kupotea huwa haupo. Kitendo hiki husababisha kazi hiyo iendelee kutumika katika jamii husika.

ii) Kutunza amali ya jamii: Mambo yanayojadiliwa katika fasihi simulizi ni mambo mbalimbali ambayo ni desturi ya jamii husika. Kitendo cha kuhifadhi kazi za fasihi simulizi husaidia kutunza amali za jamii ili ziweze kutumika kwa vizazi vijavyo.

Tanbihi

Uhifadhi Wa Fasihi Simulizi  Makala hii kuhusu mambo ya fasihi bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Uhifadhi wa fasihi simulizi kama historia yake, uenezi au maendeleo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.

Tags:

Uhifadhi Wa Fasihi Simulizi (a) KichwaniUhifadhi Wa Fasihi Simulizi (b) MaandishiUhifadhi Wa Fasihi Simulizi (c) Vinasa sautiUhifadhi Wa Fasihi Simulizi (d) Kanda za videoRuningaTarakilishiUhifadhi Wa Fasihi Simulizi Umuhimu wa kuhifadhi kazi za fasihi simuliziUhifadhi Wa Fasihi Simulizi TanbihiUhifadhi Wa Fasihi SimuliziFasihi simulizi

🔥 Trending searches on Wiki Kiswahili:

Wiki FoundationKibodiDodoma MakuluLa LigaMatiniUchaguzi Mkuu wa Tanzania, 2020Joseph Sinde WariobaIntanetiWachaggaHistoria ya TanzaniaNafsiViwakilishiNyegeUendelevuSintaksiPunyetoWabunge wa Tanzania 2020Malengo ya Kiswahili kuwa lugha ya taifaNomino za wingiWazaramoItikadiUkristoYouTubeOrodha ya Maspika wa Bunge la TanzaniaMofimuMbooShangaziUhuru wa TanganyikaUmemeUsawa (hisabati)NgonjeraNahauHifadhi ya NgorongoroYesuMoyoMafua ya kawaidaJeshi la Ulinzi la Wananchi wa TanzaniaKito (madini)Nelson MandelaMkataba wa Helgoland-ZanzibarVita vya KageraAgostino wa HippoMuda sanifu wa duniaKiunguliaFalme za KiarabuUturukiHistoria ya Kanisa KatolikiAfyaMungu ibariki AfrikaVielezi vya mahaliUzazi wa mpangoMkoa wa ArushaHadithiUwanja wa Taifa (Tanzania)Orodha ya vyama vya siasa TanzaniaWema SepetuMwanzo (Biblia)WaheheMfumo wa Msimbo wa Posta TanzaniaVirusi vya CoronaLionel MessiWayahudiVihisishiVivumishi ya kuulizaAlama ya uakifishajiUgonjwa wa kuharaFonetikiNzigeIdi AminManchester United F.C.MjasiriamaliLakabuJulius NyerereMweziMauaji ya kimbari ya RwandaAkili🡆 More