Nchi huru ni zile ambazo hazitawaliwi na nchi nyingine.
Kauli hiyo haimanishi kwamba wananchi wake ni huru, kwa sababu pengine mfalme au rais ni mwenyeji, lakini anawanyima haki zao kwa kiasi hata kikubwa (ambacho kinaitwa udikteta).
Mara nyingi nchi inajitangaza huru, halafu inatambuliwa na nchi nyingine kuwa hivi. Kama si nchi zote zinatambua rasmi uhuru wake, hali ya kisheria inabaki tata.
Siku hizi duniani kuna nchi huru karibu 200, ya mwisho kutambulika ikiwa Sudan Kusini (2011) na ndogo zaidi ikiwa Mji wa Vatikano (km2 0.44 na wakazi 600 hivi tu).
Hii haiuzii nchi kuingiliwa kwa namna moja au nyingine kama vile katika ukoloni mamboleo.
Makala hii kuhusu mambo ya siasa bado ni mbegu. Unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuongezea habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Nchi huru, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.