Jipu (kwa Kiingereza: boil au furuncle, yaani mwizi mdogo, kutoka neno la Kilatini fur, mwizi) ni tatizo la ngozi linalotokana na maambukizi ya kina ya folikuliti au maambukizi ya folikoli za nywele za jasho; mara nyingi unasababishwa na bakteria Stafilokokasi aureasi, ambayo husababisha kuvimba kwa eneo chungu lililo juu ya ngozi kutokana na mkusanyiko wa usaha na tishu mfu.
Jipu | |
---|---|
Mwainisho na taarifa za nje | |
Specialty | Dermatology |
ICD-10 | L02. |
ICD-9 | 680.9 |
DiseasesDB | 29434 |
MeSH | D005667 |
Majipu yakijikusanya huitwa kimeta.
Majipu ni vijivimbe vyekundu, ambavyo hujaa na usaha ulioko karibu na vinyweleo ambavyo ni laini, vya moto, na vinanavyouma sana. Yana ukubwa mbalimbali, kuanzia punje hadi ukubwa wa mpira wa golfu. Sehemu ya njano au nyeupe katikati ya uvimbe inaweza kuonekana wakati jipu likiwa tayari kutoa au kutokwa na usaha.
Katika maambukizi makali, mtu anaweza kuhisi homa, kuvimba tezi au mtoki, pamoja na uchovu.
Jipu linalojirudia mara kwa mara linaitwa ngozi-jipu.
Kwa kawaida bakteria, kama vile stafilokoki, ndio husababisha jipu kutokea kwenye ngozi. Ukoloni wa bakteria huanza katika vinyweleo na inaweza kusababisha seluli ya chini ya ngozi na kuvimba. Zaidi ya hayo, maiasisi inayosababishwa na wadudu wa kuruka aina ya Tumbu katika Afrika, kawaida huonesha majipu.
Sababu hatarishi za ngozi-jipu ni pamoja na bakteria katika tundu la pua, ugonjwa wa kisukari, fetma, neoplasmi s lymphoproliferative, utapiamlo, na matumizi ya madawa yanayokandamiza kingamwili.
Matatizo kawaida yanayotokana na kuambukizwa na majipu ni makovu na maambukizi au usaha wa ngozi, uti wa mgongo, ubongo, figo na viungo vingine. Maambukizi pia huweza kuenea hadi kwenye mfumo wa damu (sepsisi) na kuwa tishio kwa uhai.
Majipu yote lazima yafyonzwe ili kupona. Kunyonywa kunawezekana kwa kutumia kitambaa kilicholowa kwenye maji moto yenye kutiwa chumvi. Kuosha pamoja na kufunika jipu na krimu ya antibiotiki au mafuta ya antiseptiki (kwa jina maarufu tea tree oil) na kufunga bendeji kunasababisha kupona kwa haraka. Majipu hayastahili kufinywa au kutobolewa bila idhini ya daktari au muuguzi yeyote, kwani kunaweza kusababisha maambukizi mengine.
Katika hatari ya kutosababisha matatizo makubwa ni lazima majipu yakatwe au yafyonzwe na daktari. Hii ni pamoja na majipu makubwa yanayokaa zaidi ya wiki mbili, ama yale yanayopatikana katikati ya uso au kwenye uti wa mgongo.
Tiba ya antibiotiki linahimizwa haswa kwa kupigana na majipu makubwa yanayopatikana kwenye sehemu nyeti kama vile pua na ndani ya masikio.
Makala hii kuhusu mambo ya tiba bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Jipu kama sababu yake au mahusiano yake na mada nyingine? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Jipu, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.