Kalenda Ya Kiyahudi

Kalenda ya Kiyahudi (pia: Kalenda ya Kiebrania) ni kalenda inayotumiwa katika dini ya Uyahudi na pia nchini Israel.

Inatumiwa kupanga tarehe za sikukuu za Kiyahudi na utaratibu wa kusoma Torati kwa kila wiki.

Liturgia na sala hufuata pia mpangilio wa kalenda hiyo.

Mwaka

Kalenda hiyo inajua miaka tofauti ndani ya kipindi kilekile.

Kanuni za msingi

Kalenda ya Kiebrania ni kalenda jua-mwezi.

  • Wakati huo huo, Pasaka ya Kiyahudi inapaswa kutokea kwenye majira ya machipuo, wakati wa mwezi Aprili au mwisho wa Machi. Ilhali majira ya machipuo hufuata mwendo wa Jua, kanuni hii inafunga makadirio ya mwaka na mwendo wa Jua.
  • Hii inasababisha ulazima wa kupatanisha tofauti kati ya muda wa mwaka wa Jua (siku 365) na muda wa mwaka wa Mwezi (takriban siku 354).
  • Hapo kalenda ya Kiebrania inaongeza mwezi wa nyongeza mara saba katika kila kipindi cha miaka 19. Kwa hiyo kuna miaka ya kawaida yenye siku 354 na miezi 12. Lakini kila mwaka wa pili au wa tatu ni mwaka mrefu wenye miezi 13 na siku 384.
  • Utaratibu huo unahakikisha tarehe ya Pasaka kubaki katika majira ya machipuo ya kaskazini. Wastani wa muda wa mwaka katika kipindi cha miaka 19 ni siku 365.

Juma

Nje ya kalenda hiyo kuna utaratibu wa wiki ya siku saba zinazoendelea mfululizo, sawa na kalenda ya kimataifa. Hutumiwa kubaini siku ya Shabbat, ambayo ni siku ya kupumzika. Wiki haitegemei mwaka wa jua wala wa mwezi. Badala yake, inategemea hesabu ya siku saba ambazo zinaaminika kurudi nyakati za zamani za Babeli na kutajwa katika masimulizi ya kuumbwa kwa Dunia katika Biblia.

Siku za juma la Kiyahudi

Siku ya juma
(Kiebrania)
Tafsiri Siku inaanza kutoka kuzama kwa Jua Siku inaendelea mpaka kuzama kwa jua
יום ראשון
yom rishon
siku ya kwanza Jumamosi Jumapili
יום שני
yom sheni
siku ya pili Jumapili Jumatatu
יום שלישי
yom shelishi
siku ya tatu Jumatatu Jumanne
יום רביעי
yom revi'i
siku ya nne Jumanne Jumatano
יום חמישי
yom hamishi
siku ya tano Jumatano Alhamisi
יום ששי
yom shishi
siku ya sita Alhamisi Ijumaa
שבת
shabbat
Shabbat
(Sabato)
Ijumaa Jumamosi

Miezi

Mwezi
namba
katika Biblia
Jina la mwezi Jina la mwezi
kwa Kiebrania
Idadi
ya siku
Wakati wa mwaka Maelezo
1 Nisan נִיסָן 30 Machi - Aprili Mwezi wa Pasaka
2 Iyar אִייָר 29 Aprili- Mei
3 Sivan סִיוָן 30 Mei- Juni Mwezi wa Shavuot
4 Tammuz תַּמּוּז 29 Juni- Julai
5 Av אָב 30 Julai- Agosti Mwezi wa Tisha B'Av
6 Elul אֱלוּל 29 Agosti- Septemba
7 Tishri תִּשְׁרֵי 30 Septemba- Oktoba Mwezi wa Rosh Hashanah,
Yom Kippur na Sukkot
8 Heshvan
(au Marheshvan)
(מַרְ)חֶשְׁוָן 29 au 30 Oktoba - Novemba
9 Kislev כִּסְלֵו 30 au 29 Novemba - Desemba Mwezi wa Hanukka
10 Tevet כִּסְלֵו 29 Desemba- Januari
11 Shevat שְׁבָט 30 Januari- Februari
12 Adar אֲדָר 29 Februari-Machi Katika mwaka mrefu, mwezi wa 13 unaongezwa unaoitwa pia Adar, lakini inapewa namba; kwa hiyo katika mwaka mrefu kuna Adar I na Adar II

Siku na wiki

Katika kalenda ya Kiyahudi, siku inafafanuliwa kufuatana na Biblia ya Kiebrania: "Na ilikuwa jioni, na ilikuwa asubuhi, siku moja". Kwa sababu "jioni" inakuja kabla ya "asubuhi", siku katika kalenda ya Kiyahudi huanza jioni baada ya machweo . Ni muhimu kuhakikisha kuwa siku iliyopita imekwisha kabisa, hivyo siku mpya huanza wakati wa usiku umeanza.

Katika kalenda zinazochapishwa, tofauti hii haionekani maana hapa tarehe za kalenda ya Kiyahudi na tarehe za Kalenda ya Gregori zinazoanza usiku wa manane huonyeshwa kandokando. Ineleweka kuwa watu wanaotumia kalenda hizi wanajua utaratibu wa kuanza siku baada ya machweo. Wakati wowote sikukuu, siku ya kuzaliwa au ya kumbukumbu ikionekana kwenye kalenda iliyochapishwa, kwa kweli huanza jioni iliyotangulia, baada ya machweo.

Molad

Hesabu ya kalenda ya Kiebrania mwaka na mwezi huanza na molad inayomaanisha hilali. Molad ni neno la Kiebrania linalomaanisha "kuzaliwa". Neno hilo linamaanisha "kuzaliwa" kwa mwezi mpya kila mwezi. Kalenda ya kisasa ya Kiebrania hutumia molad iliyohesabiwa: urefu wa wastani wa muda kutoka mwezi mpya hadi mwezi mpya. Urefu wa Molad ni siku 29, masaa 12, dakika 44, sekunde 3 na nusu.

Tanbihi

Marejeo

  • Msimbo wa Maimonides (Mishneh Torah), Kitabu cha Tatu, Tolea Nane: Utakaso wa Mwezi Mpya . Ilitafsiriwa na Solomon Gandz. Yale Judaica Series Vol XI, Press University University of Yale, New Haven, Conn., 1956.
  • Bonnie Blackburn na Leofranc Holford-Strevens. Mpenzi wa Oxford kwa Mwaka: Uchunguzi wa Forodha ya Kalenda na Uhesabuji wa wakati . Vyombo vya Habari vya Chuo Kikuu cha Oxford; USA, 2000. pp 723-730.

Tovuti nyingine

Kukadiria tarehe baina ya kalenda

Tags:

Kalenda Ya Kiyahudi MwakaKalenda Ya Kiyahudi Kanuni za msingiKalenda Ya Kiyahudi JumaKalenda Ya Kiyahudi Siku za juma la KiyahudiKalenda Ya Kiyahudi MieziKalenda Ya Kiyahudi TanbihiKalenda Ya Kiyahudi MarejeoKalenda Ya Kiyahudi Tovuti nyingineKalenda Ya KiyahudiDiniIsraelKalendaKiyahudiSikukuuTareheToratiUyahudiWiki

🔥 Trending searches on Wiki Kiswahili:

KitenziNishati ya mwangaNahauPesaMbeziLahajaHadithiMajira ya baridiHadithi za Mtume MuhammadCristiano RonaldoHekaya za AbunuwasiOrodha ya matajiri wakubwa WaafrikaMmeaKitenzi kishirikishiMbuga za Taifa la TanzaniaMisemoMashariki ya KatiNdoaOrodha ya Maspika wa Bunge la TanzaniaLady Jay DeeMjombaUlumbiHeshimaIniNgeliBaraLugha ya maandishiTarbiaViwanja vya Afrika (Kwa Ukubwa)Meta PlatformsMkoa wa PwaniBiblia ya KikristoWadatogaPopoHedhiMuungano wa Madola ya AfrikaMachweoTabainiWazaramoHali ya hewaZuchuZabibuDodoma MakuluDhamiraViwakilishiTabiaTamathali za semiSamakiDamuMbwana SamattaMweziUkongaKiambishiNamba ya mnyamaWaziri Mkuu wa TanzaniaHistoria ya ZanzibarLigi Kuu Tanzania BaraUtumbo mwembambaBata MzingaFani (fasihi)Maziwa ya mamaDiamond PlatnumzKengeMkoa wa TangaMafurikoWimbo wa Jumuiya ya Afrika MasharikiJamhuri ya Watu wa ChinaPhilip Isdor MpangoVivumishiUwanja wa Taifa (Tanzania)UfisadiHistoria ya KiswahiliLugha ya taifaKifua kikuu🡆 More