Kalenda ya Kiyahudi (pia: Kalenda ya Kiebrania) ni kalenda inayotumiwa katika dini ya Uyahudi na pia nchini Israel.
Inatumiwa kupanga tarehe za sikukuu za Kiyahudi na utaratibu wa kusoma Torati kwa kila wiki.
Kalenda hiyo inajua miaka tofauti ndani ya kipindi kilekile.
Kalenda ya Kiebrania ni kalenda jua-mwezi.
Nje ya kalenda hiyo kuna utaratibu wa wiki ya siku saba zinazoendelea mfululizo, sawa na kalenda ya kimataifa. Hutumiwa kubaini siku ya Shabbat, ambayo ni siku ya kupumzika. Wiki haitegemei mwaka wa jua wala wa mwezi. Badala yake, inategemea hesabu ya siku saba ambazo zinaaminika kurudi nyakati za zamani za Babeli na kutajwa katika masimulizi ya kuumbwa kwa Dunia katika Biblia.
Siku ya juma (Kiebrania) | Tafsiri | Siku inaanza kutoka kuzama kwa Jua | Siku inaendelea mpaka kuzama kwa jua |
---|---|---|---|
יום ראשון yom rishon | siku ya kwanza | Jumamosi | Jumapili |
יום שני yom sheni | siku ya pili | Jumapili | Jumatatu |
יום שלישי yom shelishi | siku ya tatu | Jumatatu | Jumanne |
יום רביעי yom revi'i | siku ya nne | Jumanne | Jumatano |
יום חמישי yom hamishi | siku ya tano | Jumatano | Alhamisi |
יום ששי yom shishi | siku ya sita | Alhamisi | Ijumaa |
שבת shabbat | Shabbat (Sabato) | Ijumaa | Jumamosi |
Mwezi namba katika Biblia | Jina la mwezi | Jina la mwezi kwa Kiebrania | Idadi ya siku | Wakati wa mwaka | Maelezo |
---|---|---|---|---|---|
1 | Nisan | נִיסָן | 30 | Machi - Aprili | Mwezi wa Pasaka |
2 | Iyar | אִייָר | 29 | Aprili- Mei | |
3 | Sivan | סִיוָן | 30 | Mei- Juni | Mwezi wa Shavuot |
4 | Tammuz | תַּמּוּז | 29 | Juni- Julai | |
5 | Av | אָב | 30 | Julai- Agosti | Mwezi wa Tisha B'Av |
6 | Elul | אֱלוּל | 29 | Agosti- Septemba | |
7 | Tishri | תִּשְׁרֵי | 30 | Septemba- Oktoba | Mwezi wa Rosh Hashanah, Yom Kippur na Sukkot |
8 | Heshvan (au Marheshvan) | (מַרְ)חֶשְׁוָן | 29 au 30 | Oktoba - Novemba | |
9 | Kislev | כִּסְלֵו | 30 au 29 | Novemba - Desemba | Mwezi wa Hanukka |
10 | Tevet | כִּסְלֵו | 29 | Desemba- Januari | |
11 | Shevat | שְׁבָט | 30 | Januari- Februari | |
12 | Adar | אֲדָר | 29 | Februari-Machi | Katika mwaka mrefu, mwezi wa 13 unaongezwa unaoitwa pia Adar, lakini inapewa namba; kwa hiyo katika mwaka mrefu kuna Adar I na Adar II |
Katika kalenda ya Kiyahudi, siku inafafanuliwa kufuatana na Biblia ya Kiebrania: "Na ilikuwa jioni, na ilikuwa asubuhi, siku moja". Kwa sababu "jioni" inakuja kabla ya "asubuhi", siku katika kalenda ya Kiyahudi huanza jioni baada ya machweo . Ni muhimu kuhakikisha kuwa siku iliyopita imekwisha kabisa, hivyo siku mpya huanza wakati wa usiku umeanza.
Katika kalenda zinazochapishwa, tofauti hii haionekani maana hapa tarehe za kalenda ya Kiyahudi na tarehe za Kalenda ya Gregori zinazoanza usiku wa manane huonyeshwa kandokando. Ineleweka kuwa watu wanaotumia kalenda hizi wanajua utaratibu wa kuanza siku baada ya machweo. Wakati wowote sikukuu, siku ya kuzaliwa au ya kumbukumbu ikionekana kwenye kalenda iliyochapishwa, kwa kweli huanza jioni iliyotangulia, baada ya machweo.
Hesabu ya kalenda ya Kiebrania mwaka na mwezi huanza na molad inayomaanisha hilali. Molad ni neno la Kiebrania linalomaanisha "kuzaliwa". Neno hilo linamaanisha "kuzaliwa" kwa mwezi mpya kila mwezi. Kalenda ya kisasa ya Kiebrania hutumia molad iliyohesabiwa: urefu wa wastani wa muda kutoka mwezi mpya hadi mwezi mpya. Urefu wa Molad ni siku 29, masaa 12, dakika 44, sekunde 3 na nusu.
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Kalenda ya Kiyahudi, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.