'
Zuhura Othman Soud | |
---|---|
Amezaliwa | 12 Oktoba 1993 |
Majina mengine | Zuchu |
Kazi yake | Msanii |
Zuhura Othman Soud (anafahamika zaidi kwa jina lake la kisanii Zuchu; alizaliwa 22 Novemba 1993) ni mwanamuziki, mtunzi wa nyimbo na msanii wa kurekodi wa Kitanzania aliezaliwa Zanzibar. Amesainiwa chini ya lebo ya WCB Wasafi Records chini ya uongozi wa Diamond Platnumz.
Alitunukiwa tuzo ya silver play button na mtandao wa kijamii wa Youtube kwa kuwa msanii wa kwanza wa kike Afrika mashariki kwa kufikisha wafuasi zaidi ya 100,000 ndani ya wiki moja.
Katika wiki ya kusheherekea siku yake ya kuzaliwa, Zuchu alitunukiwa tuzo ya msanii bora chipukizi wa mwaka 2020 na All Africa Music Awards|AFRIMMA.
Zuchu amezaliwa kwenye familia ya wanamuziki . Ni binti wa mwanamuziki wa taarabu anayefahamika kwa jina la Khadija Kopa. Zuchu alianza kuimba akiwa na umri mdogo na baadae kushirikiana na mama yake Khadija Kopa katika wimbo unaofahamika kama Mauzauza
Zuchu alitambulika rasmi kwenye Tasnia ya muziki mnamo Aprili 2020. Mpaka sasa ana albamu moja na alichaguliwa kushiriki mashindano ya kuwania tuzo ya MTV, MAMA awards ya mwaka 2021. Kwenye mashindano hayo, Zuchu amepangwa katika kipengele cha 'best breakthrough act', anakabiliwa na ushindani kutoka kwa Elaine na Focalistic wa Afrika Kusini na Tems na Omah Lay wote kutoka Nigeria, John Blaq (Uganda) na Sha Sha (Zimbabwe). Mpaka sasa ana albamu moja na alichaguliwa kushiriki mashindano ya kuwania tuzo ya MTV, MAMA awards ya mwaka 2021. Kwenye mashindano hayo, Zuchu amepangwa katika kipengele cha 'best breakthrough act', anakabiliwa na ushindani kutoka kwa Elaine na Focalistic wa Afrika Kusini na Tems na Omah Lay wote kutoka Nigeria, John Blaq (Uganda) na Sha Sha (Zimbabwe).
Zuchu aliachia albamu ya kwanza iliyotambulika kama “ I am Zuchu “ mwaka 2020 ikiwa na nyimbo 7. Albamu yake ndiyo iliyosikilizwa na watu wengi zaidi nchini Tanzania kwa mwaka 2020 na vidio za nyimbo zake zimetazamwa na mamilioni ya watu.
Mwaka | Nyimbo | Albamu |
---|---|---|
2020 | "Hakuna Kulala" | I Am Zuchu EP |
"Nisamehe" | ||
"Kwaru" | ||
"Wana" | ||
"Raha" | ||
"Ashua"(feat. Mbosso) | ||
"Tanzania ya Sasa" | ||
"Shangilia" | ||
"Mauzauza"(feat. Khadija Kopa) | ||
"Cheche" (feat. Diamond Platnumz) | ||
"Litawachoma" (feat. Diamond Platnumz) | ||
"Hasara" | ||
"Nobody" (feat. Joeboy) | ||
2021 | "Sukari" |
Makala hii kuhusu mwanamuziki fulani bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Zuchu kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Zuchu, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.