Viunganishi ni neno au kikundi cha maneno chenye kuunganisha vipashio vya lugha ili kuunda kipashio kikubwa zaidi.
Mifano |
---|
|
Pia ni maneno yanayounganisha maneno mengine. Kiunganishi kinaweza kuunganisha neno na neno, kirai na kirai, kishazi na kishazi, sentensi na sentensi au vinginevyo.
Viunganishi havina maneno ya kupambikwa katika neno au katika kupatanishwa kisarufi ndani ya tungo. Yaani, mfano cheza, chezewa, chezeka, na kadhalika. Hayo ni maumbo ya maneno ambayo hayabadiliki.
Na, lakini, ingawa, bila, au, ila, sembuse, kwa sababu, kwa kuwa, pamoja na, ijapokuwa, tena, iwapo, labda, toka, n.k.
Kuna aina mbili za viunganishi - navyo ni:
Ama:
Viunganishi huru ni vile vinavyosimama pekee katika tungo/katikati ya vipashio vinavyoungwa. Kwa mfano: Sisi tunaimba na kucheza.
Viunganishi tegemezi ni vile ambavyo huunda kwa viambishi vya o-rejeshi vinavyowekwa katika kishazi huru kwa pamoja huunda sentensi changamano. Viambishi hivyo ni kama vile: po, ye, lo, cho n.k. Kwa mfano: Mama anayepika ni msusi.
Makala hii kuhusu mambo ya lugha bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Viunganishi kama historia yake, uenezi au maendeleo yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Viunganishi, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.