Muungano wa Madola ya Afrika ni wazo lililopendekezwa kwa ajili ya shirikisho la baadhi ya nchi zote huru 54 za katika bara la Afrika.
Wazo hili linatokana na shairi la Marcus Garvey la mwaka wa 1924, Hail, United States of Africa.
Kiongozi wa zamani wa Libya Muammar al-Gaddafi, ambaye 2009 alikuwa mwenyekiti wa Umoja wa Afrika (UA), aliendeleza wazo la Muungano wa Madola ya Afrika katika mikutano mwili ya kanda ya Afrika: wa kwanza mwezi Juni 2007 mjini Conakry, Guinea, halafu tena mnamo mwezi wa Februari mwaka 2009 mjini Addis Ababa, Ethiopia. Gaddafi awali alisukuma kuanzishwa kwa suala hili katika mkutano uliofanyika mwaka 2000 mjini Lomé, Togo, aliealeza UA kama kushindwa kwa baadhi ya mambo; Gaddafi alidai ya kwamba muungano wa kweli pekee ndiyo unaweza kutupatia uthabiti na utajiri kwa Afrika yetu. Baadhi ya viongozi wakuu wa UA walikubaliana na shirikisho lililopendekezwa, wakiamini ya kwamba ingeliweza kuleta amani katika Afrika mpya. Alpha Oumar Konaré, Rais wa zamani wa Mali na mwenyekiti wa zamani wa Tume ya Umoja wa Afrika, alizungumzia wazo hili katika sherehe za Siku ya Afrika, mnamo Mei 25, 2006.
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Muungano wa Madola ya Afrika, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.