Australia na Visiwa vya Pasifiki (pia: Oceania, Okeania, Oshania) hujumlishwa mara nyingi pamoja katika hesabu ya mabara.
Hasa watu kwenye visiwa vingi vya Pasifiki wana utamaduni wa karibu. Vilevile historia ya visiwa hivyo kabla ya kuenea kwa ukoloni imefanana katika mengi.
Hivyo mara nyingi sehemu hii ya dunia imeitwa "Bara la Kiutamaduni". Jina hili si sahihi kijiografia kwa sababu maeneo yake yako juu ya mabamba ya gandunia tofauti, kama vile bamba la Pasifiki, bamba la Australia na mengine madogo. Hata wataalamu hawapatani kuhusu mipaka ya eneo hilo.
Kwa lugha nyingi za dunia jina la "Oceania" (Okeania, Oshania) limekuwa la kawaida kutokana na neno la Kigiriki "okeanos" (kwa Kilatini: oceanus; kwa Kiingereza: ocean). Hivyo "Oceania" yamaanisha "nchi katika bahari". Ila tu hatuoni faida ya kuingiza neno hili katika lugha ya Kiswahili kwa sababu ni neno lisiloeleweka vizuri. Mara wataalamu hujadili "Oceania" kuwa visiwa vya Pasifiki pamoja na Australia; mara wanaona "Oceania" ni visiwa vile pekee bila Australia na wengine wanasema wenyewe "visiwa vya Pasifiki" ingekuwa jina zuri zaidi kama Australia haihesabiwi.
"Australasia" imekuwa jaribio tofauti la kutaja eneo, hasa kati ya wataalamu wa Australia, ila tu halipendwi na watu wengi visiwani. Hivyo imetumiwa zaidi kwa kanda la Australia na visiwa jirani pekee.
Visiwa vyote kwa pamoja (bila Australia yenyewe) hukadiriwa kuwa 7,500 vyenye eneo la nchi kavu la kilomita za mraba milioni 1.3 vilivyosambaa katika eneo la bahari la kilomita za mraba milioni 70. Takriban visiwa 2,100 vimekaliwa na watu milioni 14.9.
Eneo hili si bara kwa maana ya jiolojia. Visiwa vikubwa vya New Zealand, Guinea Mpya, Kaledonia Mpya na Tasmania ni mabaki ya bamba la Gondwana ya kihistoria. Guinea Mpya imetenganishwa na Australia kwa bahari ya Arafura isiyo na kina kirefu na wakati wa enzi ya barafu iliyopita zilikuwa kama nchi moja kwa sababu uwiano wa bahari ulikuwa chini kuliko leo.
Visiwa vingi katika Pasifiki ni milima ya volkeno inayoinuka kutoka tako la bahari hadi uso wa maji; mara nyingi zinaonyesha kasoko. Visiwa vingine vinajengwa na matumbawe yanayokua juu ya volkeno ambazo zimeishia kidogo chini ya uso wa bahari. Visiwa vingine ni atoli ambako matumbawe yamejenga tuta tumbawe kwa umbo la mviringo kuzunguka kisiwa cha kivolkeno.
Sababu ya kutokea kwa volkeno nyingi ni miendo ya gandunia katika tabaka za ganda la dunia chini ya bahari. Ngozi ya nje au ganda la dunia hufanywa na vipande mbamlimbali (=mabamba ya gandunia) vinavyoelea juu ya tabaka ya mwamba moto na kiowevu. Pale ambako vipande hivi vinagusana mara kwa joto na mwamba moto ulioyeyuka unapanda juu; pale ambao kupanda huku kunatokea haraka tunaona volkeno na hivyo kisiwa kipya kutokea. Mfano ni safu ya visiwa vya Hawaii ambavyo ni safu ya milima ya volkeno inayoanza kwenye tako la bahari, mengine inaonekana kama visiwa, mengine iko chini ya uso wa bahari.
Angalia Historia ya maeneo ya Pasifiki na Historia ya Australia
Mara nyingi kanda nne zimetofautishwa:
Maeneo yanayotajwa kwa "Melanesia" na "Australasia" huingiliana.
(Nchi huru zaonekana kwa mwandiko mzito, maeneo yaliyo chini ya nchi nyingine kwa mwandiko wa kawaida)
Jina la eneo, pamoja na bendera | Eneo (km²) | Wakazi (kadiro mnamo 1 Julai 2002) | Msongamano (watu kwenye km²) | Mji mkuu |
---|---|---|---|---|
Australasia (Australia na New Zealand) | ||||
Australia | 7,686,850 | 20,697,241 | 2.5 | Canberra |
Kisiwa cha Krismasi (Australia) | 135 | 474 | 3.5 | The Settlement |
Visiwa vya Cocos (Keeling) (Australia) | 14 | 632 | 45.1 | West Island |
New Zealand | 268,680 | 3,908,037 | 14.5 | Wellington |
Kisiwa cha Norfolk (Australia) | 35 | 1,866 | 53.3 | Kingston |
Melanesia | ||||
Fiji | 18,270 | 856,346 | 46.9 | Suva |
Sehemu za Indonesia | 499,852 | 4,211,532 | 8.4 | Jakarta |
Kaledonia Mpya (Ufaransa) | 19,060 | 207,858 | 10.9 | Nouméa |
Papua Guinea Mpya | 462,840 | 5,172,033 | 11.2 | Port Moresby |
Visiwa vya Solomon | 28,450 | 494,786 | 17.4 | Honiara |
Vanuatu | 12,200 | 196,178 | 16.1 | Port Vila |
Mikronesia | ||||
Shirikisho la Mikronesia | 702 | 135,869 | 193.5 | Palikir |
Kiribati | 811 | 96,335 | 118.8 | Teinainano |
Visiwa vya Marshall | 181 | 73,630 | 406.8 | Majuro |
Nauru | 21 | 12,329 | 587.1 | Yaren |
Visiwa vya Mariana ya Kaskazini Marekani | 477 | 77,311 | 162.1 | Saipan |
Guam (Marekani) | 549 | 160,796 | 292.9 | Hagåtña |
Palau | 458 | 19,409 | 42.4 | Melekeok |
Polynesia | ||||
Samoa ya Marekani (Marekani) | 199 | 68,688 | 345.2 | Fagatogo, Utulei |
Visiwa vya Cook (New Zealand) | 240 | 20,811 | 86.7 | Avarua |
Polynesia ya Kifaransa (Ufaransa) | 4,167 | 257,847 | 61.9 | Papeete |
Hawaii (Marekani) | 29,311 | 1,211,537 | 42.75 | Honolulu |
Niue (New Zealand) | 260 | 2,134 | 8.2 | Alofi |
Kisiwa cha Pasaka (Chile) | 163,6 | 3,791 | 23,17 | Hanga Roa |
Visiwa vya Pitcairn (Uingereza) | 5 | 47 | 10 | Adamstown |
Samoa | 2,944 | 178,631 | 60.7 | Apia |
Tokelau (New Zealand) | 10 | 1,431 | 143.1 | — |
Tonga | 748 | 106,137 | 141.9 | Nuku'alofa |
Tuvalu | 26 | 11,146 | 428.7 | Vaiaku |
Wallis na Futuna (Ufaransa) | 274 | 15,585 | 56.9 | Mata-Utu |
Total | 9,008,458 | 35,834,670 | 4.0 |
Makala hii kuhusu eneo fulani bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu eneo hilo kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Je, unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.
|
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Australia na Pasifiki, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.