Vuguvugu la Uarabuni au Vuguvuru la Kiarabu, Mchipuko wa Uarabuni (Kiarabu: الربيع العربي , kutoka kiing.
Watawala waliolazimika kutoka madarakani huko nchini Tunisia, Misri (mara mbili), Libya na Yemen. Machafuko ya kiraia yalitokea huko nchini Bahrain na Syria. Maandamano makubwa katika historia yalitokea huko nchini Algeria, Iraq, Jordan, Kuwait, Morocco na Sudan. Maandamano madogo yalitokea huko nchini Mauritania, Omani, Saudia, Jibuti, Sahara ya Magharibi na Palestina. Kulikuwa na maandamano kiasi kutoka katika nchi ambazo sio sehemu ya Ulimwengu wa Waarabu kama vile Uajemi na Israel.
Kulikuwa na mikinzano huko mipakani mwa nchi ya Israel, na maandamano ya Wakhuzestan wachache wa Kiarabu uliyotokea mwaka 2011. Huko Mali, wapiganaji wa Kituareg wakati wanarudi kutoka katika vita ya wenyewe kwa wenyewe ya Libya walichochea mzozo uliotafsiriwa kama sehemu ya "Vuguvugu la Kiarabu"" kwa upande wa nchi za Afrika Kaskazini. Mikinzano ya vikundi vya kimadhehebu iliyotokea huko Lebanoni ilionekana kuchochewa na machafuko ya Syria hivyo basi imechukuliwa kama Vuguvugu la Kiarabu.
Maandamano haya yaliambatana na kampeni za kupinga mambo mbalimbali, migomo, mashambulizi, matembezi ya miguu kwa masafa marefu, vilevile matumizi ya mitandao ya kijamiii kwa kuhamasisha na kuongeza ufahamikaji wa suala lenyewe katika jamii husika katika ulimwengu wa intaneti..
Vuguvugu nyingi za Kiarabu ziliambatana na fujo za kila aina hasa kwa kufuatia mamlaka kutaka kuzuia harakati hizi. Kwa maana hiyo, waandamanaji nao hawakubali kurudi nyuma katika suala zima la kupigania hicho walichokuwa wanakiamini. Msemo mkubwa uliokuwa unatumiwa na wagomaji katika ulimwengu wa Kiarabu ulikuwa Ash-sha`b yurid isqat an-nizam ("watu wanataka kuuangusha utawala wa kidhalimu").
Baadhi ya watafiti wamelifananisha suala hili kama zile vuguvugu za mapinduzi yaliyotokea mwaka 1989 huko Ulaya ya Mashariki au Mapinduzi ya 1848 katika majimbo ya Ujerumani.
Mfululizo wa migomo na maandamano katika Mashariki ya Kati na Afrika Kaskazini, ulianzia nchini Tunisia mnamo tarehe 18 Desemba 2010 kwa kufuatia Mohamed Bouazizi kujilipua na mafuta ya taa kwa kupinga manyanyaso na rushwa kutoka kwa maafisa wa polisi. Maandamano haya yaliamsha fujo nyengine nje ya mji ambao tukio hili limetokea na kupelekea fujo na maandamano katika nchi mbalimbali za Kiarabu.
Safu hii inaonesha baadhi ya mifululizo ya matukio yaliyotokana na vuguvugu la kwanza la Tunisia kisha kuhamia nchi nyingine za Uarabuni.
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Vuguvugu la Uarabuni, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.