Majeshi ya Ulinzi ya Kenya (kwa Kiingereza: Kenya Defence Forces, kifupi: KDF) ni vikosi vya kijeshi vya Jamhuri ya Kenya: Jeshi la Ardhi la Kenya, Jeshi la Wanamaji la Kenya, na Jeshi la Anga la Kenya huunda vikosi vya ulinzi.
Muundo wa sasa wa majeshi hayo ulifanywa mwaka 2010 na Katiba ya Kenya ya 2010. Aidha, KDF huongozwa na Sheria ya Majeshi ya ulinzi ya Kenya ya mwaka 2012 .
Rais wa Kenya ndiye Amirijeshi mkuu.
Mara kwa mara, vikosi hivyo vimehusika katika ulinzi wa amani duniani. Tume ya Waki, ilipongeza utayari wake na kuvichukulia "kuwa walitimiza wajibu wake vizuri." katika vurugu ya mwaka 2008 Hata hivyo, kumekuwa na madai makubwa ya ukiukwaji wa haki za binadamu, kama vile, wakati wa shughuli za kukabiliana na waasi katika eneo la Mlima Elgon na pia katika wilaya ya Mandera ya kati.
Kati ya mwaka 1896 hadi 1900, East African Rifles walitumika kutimiza sera za kikoloni za Uingereza. Kwa ushirikiano na Meja Cunningham wa Uganda Rifles, vita vilipangwa dhidi ya Wanandi ambao walikuwa wamepinga vikali ukoloni.
East African Rifles pia ilitumia askari Uganda Rifles kusaidia kukandamiza uasi wa vikosi vya Sudani katika Uganda.
Mwaka 1901, serikali ya Uingereza iliamua kupanga vikosi vyote katika Afrika ya Kati, Afrika ya Mashariki, Uganda na Somalia ya Kiingereza chini ya amri moja. Luteni Kanali Manning, afisa katika India Corps aliteuliwa Mkaguzi Mkuu wa vikosi vyote na kupandishwa katika ngazi ya jenerali.
Baada ya kuunganishwa kwa majeshi yote katika milki za Afrika ya Kati na ya Mashariki za Uingereza, rejimenti iliundwa tarehe 1 Januari 1902 na kuitwa "King's African Rifles". Muundo wa hilo jeshi ulikuwa kama ifuatavyo:
Tarehe 1 Aprili 1902, 3 KAR ilihamisha makao makuu kutoka Mombasa hadi Nairobi, na pamoja na 4 KAR na 5 KAR, vilikuwa vikitumiwa na serikali ya kikoloni ya Uingereza katika vita dhidi ya waliokuwa wakipinga utawala wa Uingereza.
Mwaka 1904 5 KAR kilivunjwa kwa sababu ya gharama za utunzaji na pia kwa sababu Waingereza walihisi kuwa upinzani dhidi ya utawala wao ulikuwa umedhibitiwa. Kilirejeshwa tena mwaka 1916 na kuwekwa Meru.
Mwaka 1926, 5 KAR ilivunjwa tena na rangi zao zikakabidhiwa 3 KAR zilindwe. Tarehe 1 Machi 1930 kitengo kilirejeshwa tena upya, na kurudishiwa rangi zake Nairobi. Baada ya Vita vya pili vya Dunia vikosi vyote vilitumiwa na serikali ya kikoloni dhidi ya uasi wa Mau Mau.
Katika alfajiri ya uhuru wa Kenya, Bunge la Taifa lilipitisha muswada (Miswada ya Kenya, 1963) kufanya marekebisho ya hadhi ya majeshi Kenya.
Vitengo vilivyokuwa vya King's African Rifles vilifanywa kuwa Vikosi vya Jeshi la Kenya na serikali huru ya Kenya ikapewa uwezo wa kuteua majina ya vitengo itakavyo kuanza thenashara alfajiri 12 Disemba 1963. Hivyo 3 KAR, 5 KAR, na 11 KAR vikawa 3 Kenya Rifles, 5 Kenya Rifles, na 11 Kenya Rifles mtawalia. Mabadiliko ya King's African Rifles Kenya Vikosi vya Kijeshi juu ya usiku wa manane wa tarehe hiyo ilikuwa hatua kubwa katika msingi wa leo wa vitengo vya Jeshi la Kenya.
Kati ya mwaka 1963 na mwaka wa 1967, Kenya ilipigana katika Vita vya Shifta vilivyokuwa dhidi ya Wakenya Wasomali waliotaka kuungana na jamaa zao katika Jamhuri ya Somalia.
Jioni ya tarehe 24 Januari 1964, kukosa kujitokeza kwa Waziri Mkuu wa Kenya na kuonekana kwenye televisheni, ambapo wadogo wa wanajeshi wa 11 Kenya Rifles walikuwa wakitarajia hotuba ya televisheni wakiwa na matumaini ya tangazo la kuongezewa mshahara, kulisababisha wanajeshi hao kuasi. Serikali ilifanya vikao viwili vya mahakama ya kijeshi kuwahukumu wanajeshi 43.
Baada ya uasi na kufuatia vikao vya mahakama ya kijeshi, 11 Kenya Rifles kilivunjwa. Kikosi kipya, 1 Kenya Rifles, kiliundwa kutumia wanajeshi 340 kutoka Lanet waliokuwa wamekubaliwa na Idara ya Uchunguzi wa Jinai (CID) kuwa hawakushiriki katika uasi.
Vikosi vya Uingereza vilitoka nchini tarehe 12 Disemba 1964 baada ya makubaliano yaliyofanywa tarehe 3 Juni 1964 kati ya Kenya na Katibu wa Dola kwa Uhusiano wa Jumuia ya Madola. Uingereza ilikuwa isaidie jeshi, iifadhili na itoe mafunzo kwa kikosi kipya cha Jeshi la Anga la Kenya na itengeneze Jeshi la Wanamaji la Kenya. Pia, ilikuwa itoe vitengo vya Jeshi la Kifalme la Hewani na vya Jeshi la Ardhi kuongeza usalama katika eneo la Mashariki Kaskazini. Mikopo muhimu ilikuwa ifutwe, na mali nyingi ikabidhiwe kwa Serikali ya Kenya. Kwa upande wao, ndege kutoka Uingereza zingeweza kupitia Kenya, meli za vikundi vya manowari vya Mashariki ya Mbali na vitengo vingine vya Jeshi la Kifalme la Wanamaji vingeweza kutembelea Mombasa, vifaa vya mawasiliano vingeweza kutumika hadi mwaka 1966, na vikosi vingeweza kufanya mazoezi nchini Kenya mara mbili kwa mwaka. Vikosi vya mafunzo viliendelea kutumwa nchini hadi mwaka 2015, vikisimamiwa na Kitengo cha Jeshi la Mafunzo cha Uingereza Kenya.
Timothy Parsons aliandika katika 2003:
'...Kenyatta hakuwa na wasiwasi kuhusu hali ya uaminifu wa kisiasa wa Jeshi la Kenya kwa sababu washauri wataalamu waandamizi Waingereza wa kijeshi waliitendesha kama KAR miaka ya 1960. Kufuatia masomo ya wanajeshi kutoka Lanet, maafisa wa Kiafrika walichukua amri ya uendeshaji wa vitengo vyote vikuu, lakini timu ya mafunzo ya Uingereza bado ilikuwa ikisimamia Jeshi la Kenya kwa muda mrefu wa mwongo huo. Pia, kwa kiasi kikubwa, utaratibu wa ulinzi usio rasmi uliofanywa pamoja na Uingereza ulihakikisha kwamba Kenyatta angeweza kutegemea msaada wa moja kwa moja kutoka Jeshi la Uingereza kungetokea uasi wa jeshi au jaribio la thaura.' (Imetafsiriwa)
Miezi kadhaa baada ya Brigedia Mwingereza A. J. Hardy kumkabidhi amri ya Jeshi la Kenya Brigedia Joseph Ndolo tarehe 1 Desemba 1966, ushawishi wa Uingereza ulidhihirika wakati Meja Jenerali Bernard Penfold aliteuliwa kama Mkuu wa Majenerali, nafasi mpya kama afisa mwandamizi vikosi vyote vya jeshi. Ndolo alichukua nafasi ya Penfold kama Mkuu wa Majenerali mwaka 1969, akastaafu tarehe 24 Juni 1971 baada ya kukisiwa alihusika katika njama za thaura iliyodaiwa kupangwa na Joseph Owino. Baada ya hayo, wakuu wa jeshi walikuwa wakipiga taarifa moja kwa moja kwa Waziri wa Ulinzi, James Gichuru.
Nafasi ya Mkuu wa Majenerali ilijazwa tena miaka saba baadaye wakati Daniel arap Moi alimpandisha hadhi Luteni Jenerali Jackson Mulinge kutoka Kamanda wa Jeshi hadi Mkuu wa Majenerali mwezi Novemba 1978. Mahamoud Mohamed alichukua nafasi ya Mulinge katika mwaka wa 1986, na alikuwa Mkuu wa Majenerali hadi 1996. Nafasi ya Mohamed ilichukuliwa na Jenerali Daudi Tonje, Mkuu wa Majenerali mwaka 1996-2000. (Hornsby 554)
Kutoka miaka ya 1990, Jeshi la Kenya lilijihusisha na operesheni za ulinzi wa amani za Umoja wa Mataifa. Misheni ya kwanza ya ulinzi amani ya Kenya ilikuwa Namibia na UNTAG mwaka 1989 hadi 2001. Vikosi vya Kenya vilihusika katika misheni za UNTAG, UNOSOM, UNPROFOR, UNCRO (Kroasia), UNTAES, UNOMIL, UNPREDEP katika Jamhuri ya Masedonia(1996-1999), MONUA huko Angola (1997-1999) na UNTAET huko Timor ya Mashariki (1999-2001). Mwaka 2000, wanawake walijumuishwa ndani ya vitengo vya kawaida vya jeshi na Kitengo cha Huduma ya Wanawake kuvunjwa.
Katika karne ya 21, Wizara ya Ulinzi ni sehemu ya zana za Urais. Rais huteua na hustaafisha maafisa waandamizi kutumia mamlaka yake kama Amirijeshi Mkuu. Waziri wa Ulinzi husimamia Baraza la Kitaifa la Ulinzi. Mkuu wa Majenerali ni kiongozi mtawala, mtendaji na mtoa mbinu. Kulingana na Katiba ya mwaka 2010, majeshi ya ulinzi hayawezi kutumiwa ndani mwa Kenya bila idhini ya Bunge.
Baada ya matayarisho kati ya maafisa wa kijeshi wa Kenya na Somalia mjini Dhobley mwaka 2011, vitengo vya Jeshi la Kenya vilivuka mpaka kuanzisha Operesheni Linda Nchi dhidi ya Al-Shabaab Kusini mwa Somalia. Misheni iliongozwa na majeshi ya Serikali ya Mpito ya Shirikisho ya Somalia. Mwezi Juni 2012, Majeshi ya Kenya yalijumuishwa ndani ya AMISOM.
Wizara ya Ulinzi huorodhesha vitengo na huduma zifuatazo:
Jeshi la Wanahewa la Kenya liliundwa mwaka 1966 na likaasi mwaka 1982.
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Majeshi ya Ulinzi ya Kenya, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.