Masafa ya mawimbi (pia urefu wa wimbi, mara chache lukoka; kwa Kiingereza wavelength) ni namna ya kupima na kutaja ukubwa wa wimbi.
Ni umbali kati ya sehemu za kulingana za mawimbi mawili ambayo yanafuatana, kwa mfano kati ya kilele na kilele au mabonde yao.
Mawimbi yapo kila sehemu ya mazingira asilia, kwa mfano:
Masafa ya mawimbi hutofautiana sana. Mawimbi marefu yanayoweza kutambuliwa na milango ya fahamu ya binadamu ni sauti ya besi yenye masafa ya mita 21. Sikio letu linatambua mawimbi yenye masafa kati ya milimita 17 hadi mita 21.
Mawimbi sumakuumeme yana upeo mkubwa.
Masafa ya mawimbi huwa na uhusiano wa kinyume na marudio ya wimbi. Kama marudio ya wimbi ni ya juu, masafa yake yatakuwa madogo. Vilevile kinyume, kama wimbi lina masafa makubwa, marudio yake ni madogo.
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Masafa ya mawimbi, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.