Wahan (kwa Kiing.
92% za watu wa China ni Wahan, kwa jumla ni bilioni 1.4. Kati ya watu wote duniani, 19% ni Wachina wa Han. Wachina wa Han wana viwango vya juu zaidi katika Mikoa ya Mashariki ya China, haswa katika mikoa ya Hebei, Jiangsu na Guangdong. Kuna milioni kumi kadhaa za Wahan nje ya China yenyewe, wengi wao wanaishi Asia ya Kusini-Mashariki.
Asili ya Wahan walikuwa makabila katika kaskazini ya nchi yaliyolima kwenye maeneo ya Mto Njano. Makabila hayo yalikuwa pia msingi wa milki za nasaba za kwanza.
Makabila ya Wahan yaliendelea kuenea katika China ya Kusini kwa njia ya walowezi waliotafuta mashamba mapya na uvamizi wa kijeshi. Makabila mengi ambayo hayakuwa Wahan kiasili yalipokea utamaduni na lugha ya Wahan.
Jina la "Wahan" lilianza kutumiwa wakati wa nasaba ya Han.
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Wahan, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.