Wanyaturu (au Waturu; wao hupendelea kuitwa Arimi, yaani watu wa Rimi ) ni kabila la watu wa Tanzania wanaoishi hasa katika Mkoa wa Singida.
Lugha yao ni Kinyaturu, ambayo kwa sehemu ina matamshi ya Kibantu, ingawa ina fonimu nyingi za Kikushi. Hii inaweza kuwa kwa sababu ya muingiliano wa karibu na majirani zao Wanyatunzu (watu wa kaskazini magharibi) na Wanyiramba wa maeneo ya jirani ambao ni Bantu asili.
Wana utani na Wanyiramba na Wairaqw.
Asilimia kubwa ya Wanyaturu wa sasa ni weupe: hii ni kutokana na miingiliano yao na Waarabu na kupelekea kuzaliwa machotara wengi.
Wanyaturu wengi ni Waislamu na Wakristo, kwa jumla ni wachamungu kwani ni watu wanaojua kuishika dini vizuri na kupenda ibada.
Wanyaturu wanajua sana kulinda ardhi yao kwani ni vigumu Mnyaturu kuuza ardhi yake kwa mtu ambaye si Mnyaturu.
Asili ya kabila hilo inasemekana ni nchi ya Ethiopia ambako kunasadikiwa kuwa na watu wanaotumia lugha ambayo kwa asilimia kubwa inafanana na Kinyaturu. Hudhaniwa pia kuwa Wanyaturu na Wakushi wa Ethiopia asili yao ni moja.
Walipoingia eneo la Tanganyika walichangamana na Wanyatunzu pamoja na Wasukuma, ndiyo maana mila na tamaduni zao zinashabihiana kwa kiasi kikubwa, hivi kwamba ni vigumu kumpambanua Mnyaturu na Wanyatunzu. Mpaka miaka ya 1980 Wanyaturu wengi sura na nywele zao, hasa kina mama, zilishabihiana sana na watu wa jamii ya Waoromo wa Ethiopia, na walipenda sana kujiita ni Wahabeshi. Hii ni kutokana na kuwafahamu watu wa jamii ya Kihabeshi.
Mwaka 1993 walikuwa 556,000 [1].
Ndani ya kabila hilo, kuna makundi matatu:
Kuna historia pia ya koo mbalimbali kama Unyanjoka ambao waliongoza sehemu za Wilwana. Ukoo wa Unyanjoka unaanzia Ikhangao na Ndaang'ongo, Ilongero hadi Mtinko na Mpambaa.
Unyambwa ni sehemu iliyoko Singida na inasemekana ni ukoo mkubwa sana wenye mababu wakubwa wawili: Ghambona na Hante. Ukoo huo hauvumi sana kutokana na watoto wa wazee hao kuhama Unyambwa na kwenda Iguguno, ambako lakini hawakukaa sana, wakahama tena na kuelekea hasa mikoa jirani kama Shinyanga, Tabora na Mwanza. Ni ukoo wenye watoto wengi wa kike kuliko wa kiume, na dini yao kubwa ni Uislamu.
Makala hii kuhusu utamaduni wa Tanzania bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Wanyaturu kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Wanyaturu, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.