Kirai ni kipashio cha muundo chenye neno moja au zaidi lakini ambacho hakina muundo wa kiima na kiarifu.
Muundo wa kiima na kiarifu ni ule ambao unahusisha mtendaji wa tendo na tendo linalotendwa na ambao ndio muundo wa msingi katika lugha yoyote ile. Kiima hukaliwa na nomino kama neno kuu na kiarifu hukaliwa na kitenzi kama neno kuu.
Kirai hakina muundo wa kiima na kiarifu ambao unahusisha mtendaji wa tendo na tendo linalotendwa.
Uainishaji wa aina za virai hutegemea mahusiano maalumu baina ya maneno na neno kuu, kwa mfano neno kuu katika kirai nomino ni nomino.
Kirai na tungo yaani haina mojawapo ya tungo ambayo tungo nyingine ni neno kishazi na sentensi.
Kirai kikamilishi maana labda ni jibu.
Kirai huweza kutokea upande wa kiima au kiarifu katika sentensi.
Kirai ni kikubwa kuliko neno lakini kidogo kuliko kishazi.
Makala hii kuhusu mambo ya lugha bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Kirai kama historia yake, uenezi au maendeleo yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Kirai, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.