Nguo ni kitambaa ambacho kinaweza kutumika kufunikia meza, kitanda n.k.
lakini hasa kutengenezea mavazi mbalimbali yanayovaliwa na mtu kwa ajili ya kujisitiri, kwa sababu ya kutunza heshima yake na kujikinga dhidi ya baridi, jua, mvua n.k. Ndiyo sababu mara nyingi neno "nguo" linamaanisha mavazi yenyewe.
Nguo huvaliwa kulingana na hali ya hewa na mazingira fulani, lakini pia kulingana na mitindo inayobadilikabadilika kadiri ya nyakati.
Kulingana na wanaakiolojia na wanaanthropolojia, nguo za kwanza zilikuwa manyoya, ngozi za wanyama, majani na nyasi. Uvaaji wa nguo hizi uliwasaidia binadamu haswa katika kujikinga na hewa baya, kujikinga na vumbi pamoja na dhoruba kali.
Makala hii kuhusu mambo ya utamaduni bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Nguo kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Nguo, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.