Benjamini William Mkapa (12 Novemba 1938 - 24 Julai 2020) alikuwa Rais wa awamu ya tatu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (1995-2005) na mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi, CCM.
Benjamin Mkapa | |
Muda wa Utawala 23 Novemba 1995 – 21 Decemba 2005 | |
Makamu wa Rais | Omar Ali Juma (1995–2001) Ali Mohamed Shein (2001-05) |
---|---|
mtangulizi | Ali Hassan Mwinyi |
aliyemfuata | Jakaya Kikwete |
Waziri wa Sayansi, Teknolojia na Elimu ya Juu, | |
Muda wa Utawala 1992 – 1995 | |
Rais | Ali Hassan Mwinyi |
Waziri wa Habari na Utangazaji | |
Muda wa Utawala 1990 – 1992 | |
Rais | Ali Hassan Mwinyi |
tarehe ya kuzaliwa | Ndanda, Masasi, Tanganyika | 12 Novemba 1938
tarehe ya kufa | 24 Julai 2020 Dar es Salaam |
utaifa | Mtanzania |
chama | CCM |
ndoa | Anna Mkapa |
watoto | 2 |
mhitimu wa | Chuo Kikuu cha Makerere Chuo Kikuu cha Columbia Chuo Kikuu Huria cha Tanzania |
Fani yake | mwandishi wa habari, mwanadiplomasia |
dini | Ukristo (Kanisa Katoliki) |
Mkapa alizaliwa Lupaso karibu na Masasi katika kusini-mashariki ya Tanganyika. Kuanzia 1945 hadi 1951 alsoma shule za msingi pale Lupaso na Ndanda. 1952/53 alisoma shule ya seminari ya Kigonsera akaendelea kwenye shule ya sekondari ya watawa Wabenedikto pale Ndanda hadi kumaliza O-level. 1958/59 alimaliza A-levels pale St Farncis, Dar es Salaam (leo hii Pugu Secondary). Alipokelewa kwenye Chuo Kikuu cha Makerere alipohitimu 1962.
Katika mwaka wa 1995, Mkapa alichaguliwa rais msingi wake ukiwa kampeni maarufu ya kupambana na ufisadi na kuuungwa mkono kwa nguvu na rais wa zamani Julius Nyerere . Juhudi za Mkapa za kupambana na ufisadi ni pamoja na kuumba jukwaa la wazi lililoitwa Tume ya Rais juu ya Ufisadi (Tume ya Warioba) na kuongeza msaada kwa Afisi ya Kuzuia Ufisadi.
Muhula wa pili wa miaka 5 wa Mkapa kama Rais uliisha Desemba 2005. Katika wakati wake ofisini, Mkapa alibinafsisha kampuni zilizomilikiwa na serikali akaweka sera za soko huria. Wafuasi wake walimtetea kuwa kuvutia uwekezaji wa kigeni ungesaidia kukuza uchumi. Sera zake zilipata msaada wa Benki ya Dunia na IMF na kupelekea baadhi ya madeni ya nje ya Tanzania kufutiliwa mbali.
Amekashifiwa kwa upungufu wa baadhi ya jitihada zake za kupambana na ufisadi vilevile matumizi mabaya ya fedha za umma. Utawala wake ulikuwa na matumizi sana na maposho bila kikomo. Alitumia £ 15 milioni kununua ndege ya binafsi ya kirais, vilevile karibu £ 30 milioni kwa vifaa vya angani vya kijeshi ambavyo wataalamu waliona yalizidi mahitaji machache ya majeshi ya nchi. Ilikuwa juu ya ununuzi huo wa mwisho ndipo katibu wa maendeleo ya kimataifa wa Uingereza wa wakati huo Clare Short alielezea hasira ya umma, na kusababisha yeye kujulikana kama 'Mama Radar' katika vyombo vya habari vya Tanzania.
Baada ya kutoka ofisini kwa kukamilisha mihula miwili inayoruhusiwa, Mkapa alikumbwa na shutuma nyingi za ufisadi kati yao kujipa mwenyewe na Waziri wake wa zamani wa nishati na madini Daniel Yona "Mgodi wa Makaa ya Mawe wa Kiwira" yenye faida kubwa katika Nyanda za juu za kusini mwa Tanzania bila taratibu zifuatazo. Kwa kujibinafsishia mgodi wa makaa ya mawe wa Kiwira, alivunja katiba ya Tanzania ambayo haimruhusu rais kufanya biashara yoyote katika ikulu[onesha uthibitisho].
Aliteuliwa katika Bodi ya Wadhamini ya Chuo cha Aga Khan mwezi Novemba 2007.
Nishani | Nchi | Mwaka | Ref | |
---|---|---|---|---|
Nishani ya Moyo wa Dhahabu wa Kenya (Chifu) | Kenya | 2005 | ||
Nishani ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere | Tanzania | 2011 |
Mnamo Desemba 7, 2019, alitunukiwa Nishani ya Heshima ikiwa ni kuthamini mchango wake katika kuanzisha vyuo vikuu binafsi, hivyo kukifanya Chuo Kikuu cha Iringa kuwa chuo kikuu cha kwanza binafsi nchini Tanzania wakati wa utawala wake.
Chuo Kikuu | Nchi | Shahada ya Uzamivu | Mwaka | Ref |
---|---|---|---|---|
Chuo Kikuu cha Sōka | Japan | Shahada ya Heshima | 1998 | |
Chuo cha Morehouse | Marekani | Shahada ya Heshima | 1999 | |
Chuo Kikuu Huria cha Tanzania | Tanzania | Shahada ya Heshima | 2003 | |
Chuo Kikuu ya Kitaifa cha Lesotho | Lesotho | Daktari wa Sheria | 2005 | |
Chuo Kikuu cha Kenyatta | Kenya | Daktari wa Elimu | 2005 | |
Chuo Kikuu cha Dar es Salaam | Tanzania | Shahada ya Heshima | 2005 | |
Chuo Kikuu cha Nyukasal | Ufalme wa Muungano | Daktari wa Sheria ya Kiraia | 2007 | |
Chuo Kikuu cha Rasi ya Pwani (Cape Coast) | Ghana | Daktari wa Barua | 2008 | |
Chuo Kikuu cha Makerere | Uganda | Daktari wa Sheria | 2009 |
Alitanguliwa na Ali Hassan Mwinyi | Rais wa Tanzania 1995-2005 | Akafuatiwa na Jakaya Kikwete |
Makala hii kuhusu mwanasiasa fulani bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Benjamin Mkapa kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Benjamin Mkapa, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.