Jani ni ogani ya mimea na kazi yake ya msingi ni usanisinuru na upumuaji (badiliko la gesi).
Kwa hiyo ni sehemu ya mmea iliyopo juu ya ardhi.
Umbo lake mara nyingi ni bapa na nyembamba. Ubapa unaisaidia kuwa na uso mkubwa kwa kupokea nuru nyingi iwezekanavyo, na wembamba unasaidia nuru kufikia seli ambako inatumiwa na vyembe vya viwiti kuendesha usanisinuru.
Umbo tofauti ni kama sindano. Maumbo ya jani kama sindano au miiba yanatokana na mazingira ambayo ni yabisi, ama kwa miezi kadhaa au kwa muda mrefu zaidi.
Hili ni pia umbo la majani ya kudumu ya miti inayoweza kustawi katika mazingira yenye jalidi kama vile misunobari.
Makala hii kuhusu mambo ya biolojia bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Jani kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Jani, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.