Maafa Asilia

Maafa asilia ni matukio yanayosababisha mabadiliko kwenye uso wa ardhi au angahewa ya dunia yanayoleta hasara kubwa kwa mali na maisha ya binadamu, na sababu zake ni za kiasili.

Mifano yake ni tetemeko la ardhi, banguko, kimbunga, mafuriko, tsunami, mlipuko wa volkeno au pigo la asteroidi. Matukio hayo yote si lazima yawe maafa kwa maana yakitokea mahali pasipo na wanadamu na kutosababisha hasara kwa watu basi hayaitwi "maafa".

Maafa ya asili na maafa yaliyosababishwa na binadamu

Kuna maafa mbalimbali yanayosababishwa na binadamu na sababu za kibinadamu huingiliana na maafa asilia:

  • Kwa jumla ni vita na mauaji ya vikundi fulani zilizosabisha vifo vingi
  • ajali na milipuko katika viwanda vikubwa na ghala za baruti vinaweza kuua watu na kusumisha mazingira, kwa mfano maafa ya kikemia ya Bhopal nchini Uhindi (vifo 20,000)
  • Mafuriko hutokea kutokana na kuziba njia asilia za mito na ujenzi wa nyumba katika maeneo haya ambako watu hupata hasara kama nyumba zao zinaharibika
  • maafa kutokana na ajali wakati wa kusafirisha kemikali, mafuta au baruti
  • maafa ya mazingira ambako kemikali sumu au mafuta zinasambaa (k.m. mlipuko wa BP Deepwater Horizon kwenye ghuba ya Meksiko mwaka 2010.
  • maafa ya nyuklia ambako vituo vya nyuklia vinaharibika, kwa mfano maafa ya Chernobyl (Ukraine, mwaka 1986) au maafa ya Fukushima(Japani, mwaka 2011)

Mara nyingi ni matendo ya binadamu yanayofanya tukio la kiasili kuwa maafa makubwa kwa mfano ujenzi wa makazi katika mazingira ya volkeno hai (mfano: mji wa Napoli, Italia kando ya Vesuvio) au penye mipaka ya mabamba ya gandunia inayojulikana kama vile Los Angeles, Marekani.

Tetemeko la ardhi

Tetemeko la ardhi (pia: zilizala) ni mishtuko ya ghafla kwenye ganda la dunia. Likifikia ukali fulani ni hatari hasa kwa majengo. Hatari kwa binadamu hutegemea ubora wa majengo. Vifo vingi vinaweza kutokea wakati majengo yanaporomoka na kujeruhi au kuua watu. Hata tetemeko kali haliui watu waliopo porini katika tambarare ingawa linatisha.

Nguvu ya tetemeko la ardhi hupimwa kwenye skeli ya 0-9 au zaidi.

Nguvu ya uharibifu inaweza kutofautiana sana. Kwa mfano, tetemeko la ardhi lenye nguvu ya 6.4 liliharibu mji wa Bam, Iran mwaka 2003 na kusababisha vifo vya watu zaidi ya 40,000. Lakini tetemeko huko Northridge, Kalifornia ya mwaka 1994 ilikuwa na nguvu ileile ila ni watu 60 tu waliofariki. Tofauti ilikuwa ubora wa majengo katika maeneo yaliyohusika. Ilhali takriban wanafunzi 10,000 walifariki, huko Marekani shule zote zilisimama. Athira nyingine ilikuwa hali ya huduma za dharura na muda wa mahanga kukaa chini ya kifusi cha majengo.

Maafa Asilia 
Uharibifu baada ya banguko huko Venezuela mwaka 1999.

Banguko

Banguko ni kiasi kikubwa cha mawe, ardhi, theluji au barafu kinachoanza kuteleza kwenye mtelemko wa mlimani na kuelekea bondeni. Banguko unaweza kusababishwa na tetemeko la ardhi, kuyeyuka kwa theluji mlimani au mvua kali.

Banguko kubwa la mwaka 1999 nchini Venezuela liliharibu nyumba zaidi ya 8,000 na kuua idadi ya watu isiyojulikana lakini imekadiriwa kuwa kati ya watu 10,000 hadi 30,000. Mwaka 2010 banguko kwenye mitelemko ya mlima Elgon huko Uganda likaua watu zaidi ya 100.

Kimbunga na tufani

Tufani na kimbunga ni aina za dhoruba zenye mwendo wa kuzunguka. Zinatokea hasa katika kanda la tropiki la dunia. Zinaleta upepo mkali mno pamoja na kiasi kikubwa cha mvua. Zinaweza kubomoa nyumba, kuvuta watu na hata magari hewani na kuleta mafuriko makali.

Tufani ya Katrina ya mwaka 2005 iliharibu mji wa New Orleans huko Marekani, ikasabisha vifo zaidi ya 1,200 na hasara ya mali ya takriban dolar za Marekani bilioni 108 .

Mafuriko

Maafa Asilia 
Mafuriko katika eneo la TAZARA, Dar es Salaam, Tanzania.
Maafa Asilia 
Mafuriko huko Jangwani jijini Dar es Salaam.

Mafuriko ni hali ya kuwa na maji mengi yanayofunika nchi kavu isiyo na maji kwa kawaida.

Mafuriko yanaweza kutokea

  • popote baada ya mvua kali inayoteremsha maji mengi yasiyo na njia ya kupotea, hasa baada ya kutelemka penye mlima au mtelemko
  • kando ya mto ama baada ya mvua kali au wakati wa mvua nyingi au kwenye majira ya kuyeyuka kwa theluji
  • kando ya ziwa au bahari kama upepo mkali unasukuma maji kuelekea pwani, hasa pamoja na kutokea kwa maji kujaa au bamvua

Mafuriko mara nyingi ni hatari kwa binadamu, huleta hatari kwa uhai, mali na nyumba.

Njia za kujiokoa ni pamoja na kuhama haraka sehemu za mabondeni kwenda penye miinuko au nchi ya juu zaidi. Watu waliozoea mafuriko wana mbinu za pekee kama vile kujenga vizuizi vya maji kupanda juu, kuchimba mifereji inayopeleka maji mbali au kujenga nyumba juu ya vilima wakijua hakuna njia ya kuzuia mafuriko.

Tsunami

Tsunami ni wimbi kubwa sana katika bahari inayosababishwa na tetemeko la ardhi, mlipuko wa volkeno au matokeo mengine yanayoleta mshtuko wa ghafla chini ya maji. Mshtuko huo unapita ndani ya maji si hatari sana kwa meli baharini maana haubadilishi mno uso wa bahari. Lakini pale unapokutana na nchi kavu au kufikia sehemu ambako kina cha maji kinapungua kuna wimbi kubwa linalotokea na hii ni hatari kwenye pwani ambako wimbi hilo linafikia.

Tsunami inaweza kutokea pia baada ya banguko la mtelemko mkubwa kwenye pwani ya bahari au ziwa. Kabla ya kipindi cha kihistoria kulikuwa pia na tsunami zilizosababishwa na mgongano wa gimba la angani na uso wa dunia.

Tsunami zimewahi kutokea mara nyingi duniani. Kati ya taarifa za kwanza zilizotambua uhusiano kati ya tetemeko la ardhi na tsunami ni mwandishi Thukidides wa Ugiriki ya Kale mnamo mwaka 426 KK.

Tsunami kubwa iliyotazamwa kwa msaada wa vifaa vya kisayansi ni Tsunami wa Krismasi 2004 katika Bahari Hindi iliyoua maelfu ya watu kuanzia Indonesia, Sri Lanka, Thailand na India hadi Somalia na Kenya. Ilisababishwa na tetemeko la ardhi kutokana na mwendo wa mabamba ya gandunia, hapa bamba la Burma chini ya bamba la Uhindi.

Mlipuko wa volkeno

Maafa Asilia 
Mwendo wa lava kutoka shimo la volkeno kwenye kisiwa cha Iceland, mnamo 1984.

Mlipuko wa volkeno ni kutokea vikali kwa lava na gesi kutoka ndani ya ganda la dunia. Volkeno hupatikana pale ambako vipande vya ganda la dunia vinaachana au kusukumana. Kuna pengo ambako magma joto kutoka ndani ya dunia inapanda juu kufika usoni.

Hii inaweza kutokea polepole lakini ikitokea kwa ghafla inaleta maafa katika mazingira yenye makazi ya watu.

Milipuko ya volkeno mbalimbali zinaweza kutofautiana kutegemeana na aina ya volkeno na hasa aina ya magma na lava zinazotoka nje.

  • Kuna milipuko mikali inayorusha kiasi kikubwa cha mwamba wa joto katika umbali wa kilomita kadhaa.
  • kuna milipuko inayorusha majivu ya moto inayofunika kila kitu na kuganda kuwa mwamba tena.
  • kuna milipuko ambako mto wa lava unatoka nje
  • kuna gesi za sumu zinazotoka nje na kuua kila uhai kwenye njia yake.
  • nguvu ya mlipuko inaweza kurusha miamba yenye kiasi cha kilomita za ujazo katika mazingira ya volkeno na kubadilisha uso wa dunia; mfano ni mlipuko wa mlima Krakatau huko Indonesia mwaka 1903; kisiwa cha Krakatau kilipotea kabisa.

Pigo la asteroidi

Dunia yetu inazunguka Jua letu katika anga-nje. Hapa inakutana mara kwa mara na violwa vinavyoanguka kwenye angahewa na kuonekana kama vimondo. Vingi ni vidogo, hivyo havileti hasara.

Lakini kiolwa kinachogonga Dunia kikiwa kikubwa kama asteroidi hatari ni kubwa. Migongano hiyo hutokea mara chache sana lakini sayansi imetambua ya kwamba pigo la asteroidi kubwa miaka milioni 66 iliyopita lilisababisha kuangamia kwa spishi nyingi, zikiwa pamoja na dinosauri. Pigo hilo lilirusha kiasi kikubwa cha vumbi kwenye angahewa pamoja na kusababisha milipuko ya volkeno nyingi na kuleta mabadiliko ya tabianchi kwa miaka kadhaa, hivyo kushusha halijoto duniani na kusababisha giza kwa muda mrefu.

Katika karne iliyopita kulikuwa na matukio mawili yaliyoonyesha nguvu haribifu ya violwa kutoka anga-nje:

  • mwaka 1908 kimondo kikubwa au asteroidi ndogo iligonga eneo la Tunguska huko Urusi na kuangamiza kilomita za mraba 2,000 za misitu, Kwa bahati nzuri wakati ule hapakuwa na watu katika eneo la Tunguska.
  • Mwaka 2013 kimondo kilichokadiriwa kuwa na kipenyo cha mita 17 pekee kilisababisha uharibifu kwa kulipuka juu ya mji wa Chelyabinsk nchini Urusi. Watu 1,500 walijeruhiwa, hasa na vioo vya madirisha vilivyopasuka kote mjini wakati wa mlipuko. Nyumba nyingi ziliathiriwa.

Kutambuliwa kwa hatari hii imesababisha mataifa mbalimbali kushirikiana katika mipango ya kutambua mapema violwa vinavyokaribia Dunia.

Marejeo

Viungo vya nje

Maafa Asilia 
Wikiquote ina mkusanyiko wa dondoo kuhusu:

Tags:

Maafa Asilia Maafa ya asili na maafa yaliyosababishwa na binadamuMaafa Asilia Tetemeko la ardhiMaafa Asilia BangukoMaafa Asilia Kimbunga na tufaniMaafa Asilia MafurikoMaafa Asilia TsunamiMaafa Asilia Mlipuko wa volkenoMaafa Asilia Pigo la asteroidiMaafa Asilia MarejeoMaafa Asilia Viungo vya njeMaafa AsiliaAngahewaArdhiBangukoBinadamuDuniaKimbungaMafurikoMaishaMaliMlipuko wa volkenoTetemeko la ardhiTsunami

🔥 Trending searches on Wiki Kiswahili:

NimoniaHekaya za AbunuwasiUislamu nchini São Tomé na PríncipeMvua ya maweFani (fasihi)Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa AfrikaBahari ya HindiSeduce MeMafumbo (semi)Mwanza (mji)Joyce Lazaro NdalichakoFonolojiaOrodha ya makabila ya TanzaniaLimauViwakilishi vya kumilikiHektariUtamaduniKaterina wa SienaTambikoTetekuwangaSautiFumo LiyongoMjombaMajiKarafuuKylian MbappéNchiRejistaUkooHifadhi ya NgorongoroHistoria ya AfrikaMkoa wa KageraBendera ya TanzaniaWilaya ya IlalaHasiraWanyamboJipuUajemiTawahudiJamhuri ya Kidemokrasia ya KongoTamathali za semiVivumishi vya kuoneshaKataHaki za wanyamaUhindiViwakilishi vya sifaWimboJohn Raphael BoccoArsenal FCMethaliBiasharaNdege (mnyama)TarakilishiMkoa wa SongweMkoa wa LindiKitenzi kishirikishiSomo la UchumiHisiaVirusi vya CoronaWachaggaPapa (samaki)SheriaJumba la MakumbushoNguruweOrodha ya Marais wa ZambiaDesturiViwakilishi vya urejeshiAgano la KaleWilaya ya Kinondoni🡆 More