Betlehemu (kwa Kiarabu بيت لحم, Beit Lahm) maana yake ni Nyumba ya mkate (kutoka Kiebrania בית לחם, ambapo בית = nyumba na לחם = mkate) ni mji wa Palestina, maarufu hasa kama mahali alipozaliwa Yesu Kristo kadiri ya Injili ya Mathayo na Luka.
Kadiri ya Mathayo, ndivyo ulivyotimia utabiri wa kitabu cha Mika 5:1.
Mapokeo yanataja mahali hapo katika Kanisa la Kuzaliwa lililojengwa mnamo mwaka 330 kwa amri ya Kaizari Konstantino.
Bethlehemu iko kilometa 10 hivi kusini kwa Yerusalemu, mita 765 juu ya usawa wa bahari. Kwa sasa ina wakazi zaidi ya 25,000 ambao wanategemea hasa utalii.
Inakadiriwa kuwa Bethlehemu ilianzishwa miaka 1,400 KK.
Kadiri ya Biblia, Bethlehemu ndio mji asili wa Daudi, mfalme wa pili wa Israeli na babu wa Yesu katika mfululizo wa vizazi vingi.
Makala hii kuhusu maeneo ya Asia bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Bethlehemu kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Bethlehemu, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.