Mapokeo (kutoka kitenzi kupokea) ni imani au desturi zilizorithishwa katika kundi au jamii fulani zikiwa na maana maalumu tangu zamani.
Kati yake kuna sikukuu, salamu na mavazi ambayo hayafai sana kutumika lakini yana maana kijamii, hasa kwa kumtambulisha mtu aliyeyavaa (k.mf. askari, mwanasheria, mtawa).
Mapokeo yanaweza kudumu na kubadilika kwa miaka elfuelfu, lakini yanaweza kuanzishwa na kuenea haraka.
Jina la Kiingereza "tradition" linatokana na kitenzi cha Kilatini tradere, yaani kueneza au kukabidhi.
Wazo hilo linatumika pia katika siasa, falsafa na dini, k.mf. kwa kwenda kinyume cha usasa.
Katika Ukristo, kuna mapokeo ya Kanisa yanayozingatiwa sana na baadhi ya madhehebu (hasa Wakatoliki, Waorthodoksi na Waorthodoksi wa Mashariki, lakini pia Waanglikana na wengineo) kwa sababu asili yao ni wakati wa Mitume wa Yesu, ambao ulikuwa bado wakati wa Ufunuo wa Mungu katika imani ya madhehebu hayo.
Mapokeo ya namna hiyo yanaitwa mapokeo ya Mitume kwa kuyatofautisha na mapokeo mengi yaliyotokea baadaye na ambayo yanaweza kuwa mazuri lakini pia mabayaː kwa vyovyote hayambani Mkristo kwa msingi wa imani.
Hata hivyo madhehebu mengine, hasa ya Uprotestanti, yanakataa yale yote yasiyopatikana wazi katika Biblia ya Kikristo.
Makala bado ni mbegu. Unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuongezea habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Mapokeo, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.