Visiwa vya Maluku (kwa Kiingereza: Moluccas) ni kundi la visiwa nchini Indonesia vilivyopo baina ya Sulawesi na Guinea Mpya.
Eneo lote la Maluku ni takriban kilomita za mraba 850,000 lakini nchi kavu yaani visiwa vyenyewe ambavyo ni 1,027 ni km² 74,505 pekee.
Wakazi ni takribani milioni 2.8.
Maluku ilikuwa jimbo la Indonesia hadi mwaka 1999 lilipogawiwa kuwa majimbo mawili
Visiwa vya Maluku vilijulikana kama "Visiwa vya viungo" (Spice islands) na Waarabu, Wareno na Waholanzi walishindana hapa kutawala biashara miaka 500 iliyopita hadi Maluku pamoja na visiwa vingine vya Indonesia vilipata kuwa koloni la Uholanzi.
Hadi leo kilimo cha karafuu na kungumanga ni muhimu kiuchumi pamoja na uvuvi.
Wakazi ni mchanganyiko hasa wa Wamalay pamoja na Wamelanesia. Upande wa dini Wareno walifaulu kuvuta wenyeji wengi upande wa Ukristo ilhai sehemu nyingine za Indonesia walihamia zaidi Uislamu lakini juzijuzi watu wengi walifika kutoka pande nyingine za Indonesia, wengi wao wakiwa Waislamu.
Baina ya mwaka 1999 na 2002 kulikuwa na mapigano baina ya Wakristo na Waislamu: maelfu walipoteza uhai na takriban nusu milioni walifukuzwa kutoka makazi yao.
* Severin, Tim The Spice Island Voyage: In Search of Wallace, Abacus, 1997, paperback, 302 pages, ISBN 0-349-11040-9 * Bergreen, Laurence Over the Edge of the World, Morrow, 2003, paperback, 480 pages
* Deforestation in the Moluccas
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Visiwa vya Maluku, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.