Uainishaji wa kisayansi (ing.
Inaweza kuitwa pia taksonomia.
Tangu muda mrefu watu walitambua ya kwamba wanyama au mimea mbalimbali wanafanana kati yao kwa namna moja au nyingine. Wataalamu walijaribu kupanga aina hizo kwa vikundi vyenye tabia za pamoja. Carolus Linnaeus alianza kuzipanga kwa muundo ulioeleweka kulingana na tabia za maumbile yao.
Mfumo wa Linnaeus uliendelezwa baadaye kulingana na nadharia ya Charles Darwin inayoona ya kwamba spishi mbalimbali huwa na chanzo cha pamoja, kwa hiyo inawezekana kupanga uhai wote kama mti yenye matawi makubwa, tena madogo yanayotoka kwenye makubwa.
Ujuzi wa kisasa kutokana na utafiti wa DNA ndani ya seli za viumbehai unaendelea kuongeza ujuzi wetu kwa hiyo katika mengi uainishaji ni utaalamu unaozidi kubadilika.
Kila spishi ya viumbehai inapewa jina la kisayansi lenye maneno mawili kufuatana na muundo wa uainishaji. Jina la Kisayansi linaanza kwa kutaja jenasi inayoandikwa kwa herufi kubwa, halafu neno la pili kama sehemu maalumu ya jina la spishi ile. Maneno hayo huandikwa kwa herufi za italiki. Kwa mabano hufuata jina la mtaalamu wa spishi pamoja na mwaka alioandika maelezo yake.
Kwa mfano paka anaitwa Felis silvestris (Linnaeus, 1758) na spishi hii inajumlisha paka wa porini na paka wa nyumbani.
Paka wa nyumbani anayefugwa na watu anatazamwa kama nususpishi, na nususpishi hii inaweza kutofautishwa kwa kuongeza neno la tatu "catus" kuwa "Felis silvestris catus". Hili ni jina la nususpishi ya paka wanaofugwa na watu. Nususpishi hii ina aina nyingi ndani yake, kutokana na ufugaji na uteuzi lakini zote zimo ndani ya nususpishi ileile.
Katika mabano lipo jina la mtaalamu aliyeeleza spishi hii mara ya kwanza kwa namna ya kisayansi pamoja na mwaka alipoandika. Katika mfano wa paka ni Carolus Linnaeus anayefupishwa mara nyingi kama "L.". Aliandika kitabu chake mwaka 1728.
Katika uainishaji wataalamu wamepatana jinsi ya kutumia majina kwa ngazi mablimbali. Umbo la majina haya hufuata sarufi ya Kilatini.
Ngazi | Mimea (planta) | Mwani (algae) | Uyoga (fungi) | Wanyama (animalia) |
---|---|---|---|---|
Faila | -phyta | -mycota | ||
Nusufaila | -phytina | -mycotina | ||
Ngeli | -opsida | -phyceae | -mycetes | |
Nusungeli | -idae | -phycidae | -mycetidae | |
Oda ya juu | -anae | |||
Oda | -ales | |||
Nusuoda | -ineae | |||
Familia ya juu | -acea | -oidea | ||
Familia | -aceae | -idae | ||
Nusufamilia | -oideae | -inae | ||
Kabila | -eae | -ini | ||
Nusukabila | -inae | -ina |
Makala hii kuhusu mambo ya biolojia bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Uainishaji wa kisayansi kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Uainishaji wa kisayansi, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.