Vipimo sanifu vya kimataifa (kwa ing.
Alama | Jina | Inataja |
---|---|---|
s | sekunde | wakati |
m | mita | urefu |
kg | kilogramu | masi |
A | ampea | mkondo wa umeme |
K | kelvini | halijoto |
mol | moli | kiasi cha dutu |
cd | kandela | mwangaza |
Maendeleo na matumizi ya utaratibu huo huangaliwa na Ofisi ya Kimataifa ya Vipimo.
Mfumo huu unatumia vizio saba vya kimsingi pamoja na viambishi awali 20 kwa kutaja vigawe au sehemu za vizio hivi katika mfumo wa viambishi awali vya vipimo sanifu vya SI.
Vizio vya kimsingi ni:
Vizio vyote vingine kama vile eneo, kani, shinikizo au ukinzani kiumeme vinatokana na vizio asilia.
Vipimo hivi hutumika na wanasayansi kote duniani vimeenea pia katika bishara na ufundi. Hata hivyo katika maisha ya kawaida kuna vipimo mbalimbali vinavyoweza kuwa tofauti kati ya nchi na nchi.
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Vipimo sanifu vya kimataifa, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.