Makanisa ya Bikira Maria ni maabadi ya Kikristo ambapo mama wa Yesu anaheshimiwa kwa namna ya pekee, kwa kuwa ama aliishi huko, ama alitokea ama alifanya muujiza, ama waumini wenyewe walijisikia hamu ya kuonyesha shukrani yao kwake.
Makanisa ya namna hiyo yalijengwa tangu karne za kwanza za historia ya Ukristo, hasa baada ya Hati ya Milano iliyowapa wananchi uhuru wa dini katika Dola la Roma, na siku hizi zinapatikana katika mabara yote, hata Antaktiki.
Mara nyingi ni patakatifu palipo lengo la hija hasa ya Wakristo wa madhehebu mbalimbali.
Kubwa kuliko yote ni Basilika la Bikira Maria Aparecida, Brazil, ambalo limezidiwa tu na Basilika la Mt. Petro huko Roma-Vatikano.
Makala hii kuhusu dini ya Ukristo bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Makanisa ya Bikira Maria kama historia yake, matokeo au athari zake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Makanisa ya Bikira Maria, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.