Kaaba ni jengo lenye umbo la mchemraba lililopo ndani ya msikiti mkuu wa Masjid al-Haram mjini Makka nchini Saudia.
Inatazamwa kama mahali patakatifu katika imani ya Uislamu. Waislamu huamini ni nyumba ya Mungu iliyojengwa kiasili na Adamu na baadaye na Abrahamu.
Ni lengo la safari ya hija. Kila Mwislamu mwenye uwezo anatakiwa kuitembelea angalau mara moja katika maisha yake.
Waislamu wanatakiwa kuielekea Kaaba wakati wa kusali na kila msikiti huwa na sehemu ya mihrabu inayotazama Makka. Mwelekeo huu huitwa kibla.
Makala kuhusu msikiti au sehemu nyingine za kuabudia Waislamu bado ni mbegu. Unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuongezea habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Kaaba, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.