Jengo la Empire State ni nyumba ya maghorofa mashuhuri mjini New York (Marekani) yenye umbo la mnara.
Ilikuwa jengo ndefu la dunia kwa muda wa miaka 40 tangu ukamilifu wake mwaka 1931 hadi 1972 ambako minara ya World Trade Center ilijengwa mjini New York pia. Tangu kuharibiwa kwa minara hii kwenye shambulio la 11 Septemba 2001 imekuwa jengo kubwa mjini.
Ujenzi wa Empire State Building ilianza mwaka 1930. Katika muda mfupi wa mwaka mmoja na siku 45 yaani siku 410 pekee jengo lilikamilishwa. Wakati wake ilihesabiwa kati ya maajabu ya dunia ya kisasa.
Kimo chake ni mita 381, pamoha na antena juu yake ni mita 448.7.
Katika jengo hili kuna
Empire State Building imeonekana katika filamu mbalimbali kwa mfano:
Baada ya watu kujiua kwa kuruka kutoka kilele fensi ilijengwa ya kuzungusha kilele amabako watalii wanaweza kutoka nje na kutazama mji.
Mwaka 1945 ndege ya kijeshi ya B-25 iligonga mnara kutokana na kosa la rubani wakati mawingu yalikuwa chini sana.
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Jengo la Empire State, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.