Fumbo (kutoka kitenzi kufumba; kwa Kiingereza mystery, kutoka neno la Kigiriki μυστήριον, myusterion, ambalo mzizi wake ni μύω, myuo, nanyamaza) ni jambo ambalo linanyamazisha watu kwa jinsi linavyozidi uwezo wa akili yao kuelewa.
Mbele ya fumbo, kila mmoja anaweza kulikubali kwa imani au kulikataa. Hoja haziwezi kutosha kumfanya aamue la kwanza au la pili.
Hata hivyo, baada ya kuamini, pengine mtu anaweza kutumia akili na hoja ili kujaribu kuelewa na kueleza kwa kiasi fulani fumbo lenyewe, mradi kwanza amelikubali kama limefunuliwa na Mungu.
Ufafanuzi huo unategemea hasa maandiko matakatifu ya dini husika, kwa mfano Biblia kwa Wakristo.
Makala hii kuhusu mambo ya dini bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu mada hii kama historia yake au uenezi wake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Fumbo, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.