Demokrasia (kutoka neno la Kigiriki δημοκρατία, dēmokratía, maana yake utawala wa watu: δῆμος, dêmos, maana yake watu na κράτος, krátos, maana yake utawala) ni aina ya serikali.
Neno hilo lilitumika kuanzia karne ya 5 KK kuelezea mtindo wa utawala uliotumika katika Athene na miji mingine kadhaa ya Ugiriki, kinyume cha ἀριστοκρατία, aristokratía, "utawala wa masharifu".
Kwenye demokrasia watu fulani wa jamii wanamchagua kiongozi wao.
Kuna njia nyingi za kufanya hivi, lakini mchakato kamili kwa kawaida huitwa kushikilia uchaguzi.
Vyama vya siasa huhusika na masuala ya siasa. Yaonekana kwamba yaweza kuwa rahisi kuwa na chama cha kisiasa. Chama kitakachoshinda uchaguzi kitamchagua kiongozi kinayemtaka.
Demokrasia ni mfumo wa serikali ambapo wananchi wote ni sawa mbele ya sheria na wanashiriki katika kufanya maamuzi ya kitaifa juu ya masuala ya umma. Wakati mwingine wananchi hushiriki moja kwa moja - hii ina maana kwamba wao hupiga kura moja kwa moja kwenye masuala kama vile sheria na katika chaguzi. Wakati mwingine huwakilishwa na viongozi wao waliowachagua.
Ni utawala wa watu, na watawala hutawala kwa ridhaa ya watu.
Kwa hiyo kwa kifupi Demokrasia ni mfumo unatoa fursa ya madaraka kwa umma moja kwa moja au kutokana na uwakilishi.
Abraham Lincoln, Rais wa 16 wa Marekani, alisema Demokrasia ni serikali ya watu/mfumo wa utawala wa watu, kwa ajili ya watu na unaotokana na watu. Watu wanaunda serikali.
Makala hii kuhusu mambo ya siasa bado ni mbegu. Unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuongezea habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Demokrasia, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.