Afrika hapo awali lilikuwa jina la jimbo la Dola la Roma katika mwambao wa Mediteranea huko Afrika Kaskazini miaka 146 KK - 698 BK.
Eneo lake lilikuwa takriban Tunisia ya kaskazini pamoja na pwani ya Libya ya magharibi na Algeria ya mashariki.
Jimbo lilikuwa maarufu kama "ghala ya ngano" ya Roma.
Watu wa Afrika ya Kaskazini kiasili walikuwa hasa Waberber.
Miji muhimu ilikuwa Karthago na Leptis Magna.
Bara la Afrika limepokea jina lake kutoka jimbo hili. Waarabu waliendelea kutawala eneo lake kwa jina la jimbo la Ifriqiya ambalo ni matamshi yao ya "Afrika".
Neno "Afrika" limetokana na lugha ya Kilatini ya Roma ya Kale ambalo Waroma kwa jina hilo (Africa Proconsularis) hawakumaanisha bara lote bali eneo la Tunisia ya leo na kandokando yake upande wa Libya na Algeria.
Inasemekana asili ya jina hilo ni kabila la "Afrig" lililoishi sehemu zile, lakini kuna pia maelezo mengine tofautitofauti.
Wakati huo Wagiriki wa Kale walitumia zaidi jina la Libya kwa ajili ya nchi kusini kwa Bahari ya Mediteraneo.
Maeneo ya ndani kuelekea kusini mara nyingi yaliitwa kwa jina la "Ethiopia" linalomaanisha labda nchi ya watu weusiweusi (kwa Kigiriki "aithiops": aliyechomwa na jua).
Katika ramani za kale kutoka Ulaya maneno yote matatu ya "Afrika", "Lybia" na "Ethiopia" yanapatikana yakitumika kama jina la bara zima. Jina la "Afrika" limekuwa la kawaida kuanzia karne ya 16 BK.
Makala hii kuhusu mambo ya kihistoria bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Afrika ya Kiroma kama enzi zake au matokeo yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Afrika ya Kiroma, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.