Injili ya Mathayo ni kitabu cha kwanza katika orodha ya vitabu vya Agano Jipya katika Biblia ya Kikristo.
Huhesabiwa kati ya Injili Ndugu pamoja na Marko na Luka, kwa sababu inafanana nazo kwa kiasi kikubwa; hasa inatumia asilimia 80 ya maandiko ya mwinjili Marko.
Kama vitabu vingine vyote vya Biblia, hiki pia kinatakiwa kisomwe katika mfululizo wa historia ya wokovu ili kukielewa kadiri ya maendeleo ya ufunuo wa Mungu kwa binadamu.
Katika matoleo ya Biblia kichwa cha kitabu ni "Injili kama ilivyoandikwa na Mathayo" lakini kichwa hiki si sehemu ya toleo asili la Kigiriki.
Ingawa Injili yenyewe haimtaji mwandishi wake, kuanzia Papias (mnamo mwaka 130) Mtume Mathayo ametajwa kama mwandishi wa misemo ya Yesu Kristo kwa lugha ya Kiebrania.
Wataalamu wanajadili kiasi gani maandishi yake yamechangia Injili hii jinsi ilivyo.
Wakati wa kutolewa unaaminiwa na wataalamu wengi wa kisasa ilikuwa kati ya mwaka 80 na 90, yaani baada ya hekalu la Yerusalemu kubomolewa, tena baada ya Wayahudi kuwatenga wenzao waliomuamini Yesu.
Mathayo anakazia kuwa Yesu wa Nazareti ndiye Masiya aliyetangazwa na manabii wa Agano la Kale. Kwa sababu hiyo Mathayo anaripoti maneno ya Agano la Kale mara kwa mara ili kuthibitishwa yametimia katika maisha ya Yesu.
Tabia hii inachukuliwa kuthibitisha maelezo ya kwamba Injili hii ililenga Wakristo ambao walikuwa Wayahudi na kutumia lugha ya Kigiriki.
Mathayo anakazia pia mafundisho ya Yesu ilhali Marko anaeleza zaidi matendo yake.
Injili hii inaanza kwa kuorodhesha mababu wa Yesu. Kutokana na mwanzo huu, vizazi vya baadaye vilimpa Mwinjili Mathayo nembo la mwanamume au malaika akichora habari za Biblia.
Makala hii kuhusu mambo ya Agano Jipya bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Injili ya Mathayo kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Injili ya Mathayo, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.