Visiwa vya Faroe (kwa Kifaroe: Føroyar - Visiwa vya kondoo) ni funguvisiwa ya Atlantiki ya Kaskazini kati ya Iceland, Uskoti na Norwei.
Visiwa vya Faroe |
---|
Wakazi wa kwanza walikuwa wamonaki kutoka Ireland.
Kati ya miaka 1035 na 1814 visiwa vilikuwa chini ya Norwei. Ndipo vilipotolewa kwa Denmark.
Kufikia mwanzo wa mwaka 1540 wakazi walikuwa wamejiunga na Matengenezo ya Kiprotestanti na kuwa Walutheri.
Kuanzia mwaka 1948 ni jimbo la nje la ufalme wa Denmark lenye madaraka ya pekee ya kujitawala. Visiwa vinaendesha shughuli zao isipokuwa siasa ya nje, jeshi na mambo ya mahakama ni chini ya serikali kuu. Hali ya kisiasa ndani ya Denmark inalingana na Greenland ambayo pia ni jimbo la nje la Denmark linalojitawala kwa kiwango kikubwa.
Visiwa vya Faroe viliamua kutoingia katika Umoja wa Ulaya pamoja na Denmark. Kumbe vimeunda umoja wa forodha na Iceland.
Wakazi wengi wana asili ya Skandinavia upande wa baba (87%) na ya Wakelti upande wa mama (84%).
Lugha rasmi ni Kifaroe, lugha ya Kigermanik ya Kaskazini karibu na Kiiceland.
Hadi leo 84.1% za wakazi ni Walutheri na madhehebu yao ndiyo dini rasmi.
Makala hii kuhusu maeneo ya Ulaya bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Visiwa vya Faroe kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Visiwa vya Faroe, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.