Reli ya Tanganyika (pia: Reli ya Kati) ilikuwa jina la njia ya reli kuanzia Dar es Salaam kwenda Kigoma kwenye Ziwa la Tanganyika iliyojengwa katika miaka 1905 hadi 1914 zamani za koloni la Afrika ya Mashariki ya Kijerumani.
Majina mengine yaliyotumika yalikuwa kwa Kijerumani "Mittellandbahn", baadaye kwa Kiingereza "Central line" (Reli ya Kati), au "Tanganjikabahn" (kwa Kiingereza Tanganyika Railway).
Reli hii ilikuwa na urefu wa kilomita 1245.4 ikitumia geji (upana wa njia) ya mita 1.
Baada ya mwisho wa ukoloni wa Kijerumani eneo la Tanganyika lilitawaliwa na Uingereza kama eneo la kudhaminiwa la Shirikisho la Mataifa. Katika kipindi hicho Reli ya Tanganyika iliongezwa njia ya kando kutoka Tabora kwenda Mwanza. Tangu mwaka 1977 njia hii imetawaliwa na Shirika la Reli Tanzania (Tanzania Railways Limited - TRL).
Njia ya reli hii inaanza Dar es Salaam ikipitia Morogoro, Dodoma na Tabora hadi kufika Kigoma.
Kuna njiapanda ambako njia ya kati inaunganishwa na njia za kando.
Kilomita | Kituo muhimu | Mwungano na njia nyingine |
---|---|---|
0 | Dar es Salaam | |
79.7 | Ruvu | |
82.9 | Ruvu Junction | njia ya Tanga - Arusha |
203 | Morogoro | |
289.5 | Kilosa | kwenda njia ya TAZARA |
455.5 | Dodoma | |
585.6 | Manyoni | njia ya Singida |
840.5 | Tabora | njia ya Mwanza |
936.7 | Kaliua | njia ya Mpanda |
1245.4 | Kigoma |
Reli ya Tanganyika (pia: Reli ya Kati) ilikuwa jina la njia ya reli kuanzia Dar es Salaam kwenda Kigoma kwenye Ziwa la Tanganyika iliyojengwa katika miaka 1905 hadi 1914 zamani za koloni la Afrika ya Mashariki ya Kijerumani.
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Reli ya Tanganyika, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.