Mwanafarasi (Equuleus kwa Kilatini na Kiingereza) .
ni jina la kundinyota ndogo ya nusutufe ya kaskazini ya Dunia.
Mwanafarasi linapakana na mkundinyota jirani ya Dalufnin (Delphinus), Dalu au Ndoo (Aquarius), Farasi (Pegasus) na Mbweha (Vulpecula). Kundinyota hii iko karibu na nyota angavu sana ya Tairi (Altair).
Mwanafarasi dogo sana kwa hiyo hatuna habari ya matumizi yake na mabaharia Waswahili. Lilitajwa tu na Klaudio Ptolemaio kama „sehemu ya Farasi“ ilichorwa kama kichwa cha farasi tu kando la farasi kubwa la Pegasus. Kunda dalili ya kwamba ilibuniwa na Hipparchos wa Nikaia
Waarabu waliipokea hivi na Wagiriki.
Equuleus - Mwanafarasi ni kati ya makundinyota yaliyotajwa tayari na Klaudio Ptolemaio katika karne ya 2 BK. Iko pia katika orodha ya makundinyota 88 ya Umoja wa kimataifa wa Astronomia kwa jina la Equuleus. Kifupi chake rasmi kufuatana na Ukia ni 'Equ'.
Jina la (Bayer) | Namba ya Flamsteed | Jina (Ukia) | Mwangaza unaoonekana | Umbali (miaka nuru) | Aina ya spektra |
---|---|---|---|---|---|
α | 8 | Kitalpha | 3,92m | 186 | G0 III |
δ | 7 | Delta Equulei | 4,49m | 55 |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Mwanafarasi (kundinyota), which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.