Bahari ya Kiarabu (kwa Kiarabu: بحر العرب bahr al-arab) ni sehemu ya kaskazini ya Bahari Hindi iliyopo baina ya Bara Arabu na Bara Hindi.
Eneo lake ni takribani kilomita za mraba 4,82,000 ilhali kina kirefu ni mita 4,652..
Upande wa kaskazini inapakana na Pakistan na Iran, upande wa magharibi na Omani, Yemen na Somalia, upande wa mashariki na Uhindi. Ghuba ya Aden iko upande wa magharibi-kusini na hapa mlangobahari wa Bab el Mandeb ni njia ya kuingia Bahari ya Shamu. Ghuba ya Oman inaunganisha na Ghuba ya Uajemi.
Mpaka wa kusini ni mstari baina ya rasi ya Bara Hindi hadi Rasi Guardafui kwenye Pembe la Afrika.
Mto mkubwa unaoishia humu ni mto Indus.
Visiwa si vingi, ni pamoja na Sokotra (Yemen), Masirah (Omani), Lakshadweep (Uhindi) na Astola (Pakistan).
Makala hii kuhusu maeneo ya Asia bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Bahari ya Kiarabu kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Bahari ya Kiarabu, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.