Guba ya Aden ni mkono pana wa Bahari Hindi kati ya Somalia upande wa kusini na Rasi ya Uarabuni upande wa kaskazini.
Inaanza kwenye sehemu ya Bahari Hindi iitwayo pia Bahari Arabu na kuelekea kwa mlango wa bahari wa Bab el Mandeb unaoiunganisha na Bahari ya Shamu.
Ghuba hii ina urefu wa kilomita 1,000 na upana wake ni kati ya 150 km hadi 440 km. Kimo cha maji hufikia urefu wa mita 3,748. Imepakana na nchi za Yemen, Somalia (au Somaliland) na Jibuti.
Mabandari muhimu zaidi ni Aden nchini Yemen, Berbera nchini Somalia na mji wa Jibuti nchini Jibuti.
Kuna funguvisiwa viwili:
Kijiolojia ghuba ya Aden ni sehemu ya kaskazini ya Bonde la Ufa la Afrika ya Mashariki linaloendelea hapa chini ya uso wa bahari.
Siku hizi ghuba hii ni kati ya njia za bahari hatari kwa usafiri kwa meli kwa sababu ya maharamia wenye vituo vya hasa Somalia lakini pia Yemen. Manowari za kimataifa zinajaribu kulinda eneo hili.
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Ghuba ya Aden, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.