Kijiji maana yake kwa Kiswahili ni mji mdogo.
Kadiri ya mazingira, kinaweza kuwa na wakazi mia chache hadi elfu chache.
Kwa kawaida vinapatikana mbali na miji, mashambani au porini kabisa.
Kiasili idadi kubwa ya wanavijiji ni wakulima na asilimia ya wakazi wanaofanya kazi tofauti ni ndogo. Kihistoria watu wengu duniani waliishi katika vijiji na kujitegemea humo.
Katika nchi zilizoendelea kilimo kimebadilika na wakulima wamekuwa wachache wanaoendelea kulima mashamba yote kwa msaada wa mashine. Hapo wakazi wengine wa kijiji wanafanya kazi nje wakisafiri kila siku hadi mahali pa ofisi, duka au kiwanda.
Siku hizi kwenye Dunia kwa jumla wanadamu wanaoishi katika miji mikubwa ni wengi kuliko wale wanaoishi bado vjijini.
Katika nchi nyingi kijiji ni pia ngazi ya chini ya utawala wa nchi. Kwa mfano nchini Tanzania kijiji kinajumlisha vitongoji kadhaa na pamoja a vijiji vingine inafanya kata.
Makala bado ni mbegu. Unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuongezea habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Kijiji, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.