Ukanda Wa Kuiper

Ukanda wa Kuiper (kwa Kiingereza Kuiper belt) ni eneo la mfumo wa jua letu nje ya obiti ya sayari Neptuni lililopo kwenye umbali wa vizio astronomia) kati ya 30 - 50 kutoka jua.

Ukanda Wa Kuiper
Ugawaji wa magimba ya ukanda wa Kuiper (nukta kijani) *Nyekundu = Jua *Buluu-kijani = Sayari jitu za gesi *Kijani = Ukanda wa Kuiper *Kichungwa = magimba mbalimbali yaliyotawanyika *Dhambarau = Watroia wa Mshtarii *Njano = Watroia wa Neptuni Namba zinadokeza umbali kwa AU

Ukanda huu una umbo la wingu wa mviringo wa magimba ya angani; mengi yao ni madogo, machache makubwa kwa hiyo ukubwa kati ya vumbi na mawe hadi asteroidi na pia sayari kibete,

Ukanda wa Kuiper hufanana na ukanda wa asteroidi ulipo kati ya obiti za Mirihi (Mars) na Mshtarii (Jupiter) lakini ni kubwa zaidi. Upana wake ni mara 20 na unene wake mara 20-200.

Magimba ndani yake ni hasa aina mbalimbali za barafu kutokana na elementi zilizoonekana kama gesi katika mazingira ya dunia kama vile methani, amoni au maji. Wataalamu wanaamini leo ya kwamba chanzo hasa cha magimba ni mchakato wa kutokea kwa mfumo wa jua letu na kuzaliwa kwa sayari. Katika maeneo ya ndani ya mfumo wa jua mata ilijikusanya kutokana na graviti kuwa ama jua lenyewe au sayari. Hapa nje masi za magimba hazikutosha kuyavuta magimba mengine ili sayari kubwa itokee.

Hata hivyo kuna sayari kibete tatu zilizogunduliwa hadi sasa katika ukanda wa Kuiper ambazo ni Pluto, Haumea na Makemake.

Kuna pia nadharia ya kwamba miezi kadhaa katika mfumo wa jua letu ina asili yake katika ukanda wa Kuiper. Mifano ni Triton ya Neptuni na Phoebe ya Zohali. Miezi hii inaaminiwa ilijijenga katika ukanda wa Kuiper lakini ilivutwa ndani ya mfumo wa jua na kukamtwa na graviti ya sayari hizo.

Ukanda wa Kuiper uligunduliwa mwaka 1992 lakini iliwahi kutabiriwa na wataalamu mbalimbali pamoja na Gerard Kuiper.

Hadi sasa kuna takribani magimba 1,000 yaliyogunduliwa kwa uhakika lakini inaaminiwa ya kwamba jumla ya magimba unaweza kufikia idadi ya malakhi au mamilioni.

Ukanda Wa Kuiper Makala hii kuhusu mambo ya sayansi bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Ukanda wa Kuiper kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.

Tags:

JuaKiingerezaMfumo wa jua letuNeptuniObitiSayariUmbaliVizio astronomia

🔥 Trending searches on Wiki Kiswahili:

WashambaaMawasilianoOrodha ya mito nchini TanzaniaFasihiAlfabetiBendera ya KenyaIsraeli ya KaleOrodha ya makabila ya TanzaniaBiolojiaTendo la ndoaBunge la TanzaniaUsafi wa mazingiraHarmonizeMatumizi ya LughaBiblia ya KikristoMkoa wa SongweMkwawaBloguMkopo (fedha)Vitamini CUlumbiBidiiUtumbo mwembambaWilaya ya ArushaMatiniUhifadhi wa fasihi simuliziMmeaRufiji (mto)Orodha ya milima mirefu dunianiNuktambiliRupie ya Afrika ya Mashariki ya KijerumaniMoyoVichekeshoMarie AntoinetteBahari ya HindiMchwaMfumo katika sokaSah'lomonWanyaturuMilango ya fahamuHerufiTarafaTafakuriTanganyikaNomino za wingiVidonge vya majiraFalsafaAdolf HitlerLigi Kuu Tanzania BaraMkoa wa RuvumaHoma ya matumboKonyagiKoroshoBawasiriVita Kuu ya Pili ya DuniaHifadhi ya mazingiraVivumishi vya idadiMadhara ya kuvuta sigaraShangaziKiazi cha kizunguMtakatifu MarkoDalufnin (kundinyota)Wilaya ya KinondoniMbeya (mji)Vivumishi vya kumilikiKiingerezaUgonjwa wa uti wa mgongoVielezi vya idadiWamasaiMkoa wa KigomaSteve MweusiKanga (ndege)MshororoNgamiaInshaUNICEFOrodha ya majimbo ya Marekani🡆 More