Kizio astronomia (ing.
Kinalingana na umbali wa wastani kati ya dunia na jua.
Urefu wake ni mita 149,597,870,691 au kwa kifupi takriban kilomita milioni 150. Umbali huu ni sawa na wastani wa umbali kutoka kitovu cha Dunia hadi kitovu cha Jua.
Vipimo vilivyo kawaida duniani kama kilomita vinaweza kutumiwa katika astronomia lakini vinaleta namba kubwa mno. Hivyo astronomia imebuni vipimo vyake vinavyorahisisha kutaja umbali wa magimba katika anga-nje. Mara nyingi astronomia hutumia kipimo cha mwakanuru kwa kupima umbali katika ulimwengu. Lakini kwa umbali za karibu zaidi jinsi ilivyo ndani ya mfumo wa Jua letu kizio astronomia kimechaguliwa.
63,241.077 vizio astronomia vinafanya mwakanuru 1.
Jina la sayari / gimba | Umbali hadi jua kwa vizio astronomia |
---|---|
Utaridi (Mercury) | 0.39 |
Zuhura (Venus) | 0.72 |
Dunia | 1 |
Mirihi (Mars) | 1.52 |
Mshtarii (Jupiter) | 5.2 |
Zohari (Saturn) | 9.58 |
Uranus | 19.23 |
Neptuni | 30 |
Ukanda wa Kuiper | kuanzia 30 |
Pluto | 39 |
Chombo cha angani kilichofika mbali hadi sasa ni "Voyager 1". Mwaka 2019 kilipita vizio astronomia 145 kutoka Jua, nje ya obiti ya Pluto na ukanda wa Kuiper.
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Kizio astronomia, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.