Laurenti (kwa Kilatini Laurentius; Valencia au Huesca, Hispania, 225 hivi - Roma, Italia, 10 Agosti 258) alikuwa shemasi mkuu wa Kanisa la Roma hadi alipouawa kwa kubanikwa kutokana na imani yake katika Yesu.
Laurenti alikuwa msimamizi wa mali ya Kanisa la Roma iliyotumiwa kwa ajili ya kuwasaidia maskini. Serikali ya Kaisari Valerian iliwahi kumwua askofu wa Roma Sixtus II ikadai sasa Laurenti atoe hazina yote ya Kanisa kwa serikali ya Kaisari katika muda wa siku tatu. Laurenti alitumia muda huo kugawa pesa zote kwa maskini.
Akitamani kushiriki kifodini cha askofu wake, anavyosimulia Papa Leo I, siku alipotakiwa kufika mbele ya afisa wa serikali kukabidhi pesa alikuja pamoja na kundi kubwa la maskini, wagonjwa, walemavu, vipofu, wenye ukoma, wajane na mayatima. Halafu kwa dhihaka alimwambia akida, "Hao ndio hazina ya Kanisa". Akida alimtesa na kumfunga kwenye nondo za chuma juu ya moto hadi alikufa. Inasemekana ya kwamba Laurenti alivumulia mateso kimyakimya akisema mwishoni, "Ewe mtu maskini, kwangu moto huu umepoa lakini kwako utaleta maumivu ya milele". Alizikwa katika shamba la Mungu la Verano ambalo mpaka leo linaitwa jina lake.
Anaheshimiwa na madhehebu mbalimbali ya Ukristo kama mtakatifu mfiadini, hasa siku ya kifodini chake.
Makala hii bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Laurenti Mfiadini, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.