Hifadhi ya Katavi ni moja ya hifadhi za taifa iliyoundwa mwaka 1974.
Iko juu ya uwanda mpana wa mafuriko magharibi mwa Tanzania katika mkoa wa Katavi na mkoa wa Rukwa. Hifadhi hiyo inazo takribani kilomita za mraba 4,471 (maili za mraba 1,726) katika eneo hilo, ambayo inakuwa ni hifadhi ya tatu kwa ukubwa nchini Tanzania.
Ni hifadhi ya mbali sana ambayo hutembelewa mara kwa mara kuliko viwanja vingine vya Tanzania. Hifadhi hiyo inahusisha mto Katuma na msimu wa Ziwa Katavi na Ziwa Chada.
Hifadhi hii inasifika kwa:
Pia wanyama kama simba na chui hawana shida ya mawindo kwani katika himaya yao kuna makundi ya swala, nyamela topi wa miguu mieupe, pundamilia na nyati.
Kuna aina zipatazo 400 za ndege waliozagaa katika miti ya acacia, kingo za mto, mabwawa na makundi kadhaa ya mwari (pelicans) yanayoambaa ziwani. Ni kawaida kuyaona makundi makubwa ya tembo yakila majani katika mabwawa, huku miili yao ikiwa imefunikwa na maji na magugu.
Majarida ya hifadhi za Taifa Tanzania
Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Katavi bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu eneo hilo kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. Tafadhali usiingize majina ya maafisa au viongozi wa sasa maana wanabadilika mno. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Hifadhi ya Katavi, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.