Adama Barrow (*16 Februari 1965) ni rais wa Gambia na mwanasiasa wa chama cha United Democratic Party.
Jinsia | mume |
---|---|
Nchi ya uraia | Gambia |
Jina katika lugha mama | Adama Barrow |
Jina halisi | Adama |
Jina la familia | Barrow |
Tarehe ya Kuzaliwa | 15 Februari 1965 |
Mahali alipozaliwa | Mansajang Kunda |
Mwenzi | FatoumatA BAH |
Lugha zinazozungumzwa, zilizoandikwa au zilizotiwa sahihi | Kifulfulde-Borgu, Kiingereza |
Kazi | politician, treasurer |
Nafasi ilioshikiliwa | President of the Gambia |
Mwanachama wa chama cha siasa | United Democratic Party, National Reconciliation Party, National People's Party |
Candidacy in election | 2016 Gambian presidential election |
Dini | Uislamu |
Tuzo iliyopokelewa | Order of the Republic of The Gambia |
Barrow alizaliwa katika kijiji cha Mankamang Kunda karibu na Basse. Alisoma shule ya msingi Koba Kunda na shule ya sekondari Crab Island mjini Banjul. Baadaye alipata nafasi kwenye Muslim High School ya Banjul.
Baada ya kufaulu aliajiriwa na kampuni ya Alhagie Musa & Sons na akapandishwa cheo hadi kuwa muuzaji mkuu.
Baada ya mwaka 2000 Barrow alihamia London aliposoma uchumi. Wakati huu alifanya kazi ya usiku kama mlinzi wa nyumba kwa kujipatia riziki.
Baada ya kurudi Gambia mwaka 2006 alianzisha kampuni ya Majum Real Estate akawa meneja mkuu hadi sasa.
Mwaka 2016 Barrow alichaguliwa kuwa mgombea wa urais katika mkutano wa vyama 7 vya upinzani.
Tarehe 2 Desemba 2016 Barrow alishtusha taifa kwa kumshinda Yammeh katika uchaguzi wa urais kwa kupata kura 263,000 au asilimia 45 za kura zote dhidi ya kura 212,000 au asilimia 36 kwa rais Yahya Jammeh. Mgombea wa tatu Mama Kandeh alipata asilimia 17.
Kwanza Rais Yahya Jammeh alikubali kushindwa hata kabla ya tangazo rasmi la matokeo, lakini siku nane baadaye alianza kung'ang'ania madaraka.
Kufuatana na katiba rais Adama Barrows alitakiwa kuapishwa takribani siku 60 baada ya uchaguzi., lakini tarehe 9 Disemba 2016 rais Jammeh alitangaza ya kwamba hakubali matokeo akitaka uchaguzi mpya.
Tarehe 19 Januari 2017, rais mteule aliapishwa katika ubalozi wa Gambia huko Dakar, halafu wanajeshi wa Senegal, Nigeria na Ghana walivamia nchi ili kumuondoa madarakani kwa idhini ya Umoja wa Mataifa.
Mnamo Novemba 2021, Adama Barrow alitangaza kugombea tena nafasi ya uraisi mwaka 2024.
Makala hii kuhusu mwanasiasa fulani bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Adama Barrow kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Adama Barrow, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.