Ngeli 4:
Sifongo-bahari | ||||||
---|---|---|---|---|---|---|
Sifongo kijani (Aplysina aerophoba) | ||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||
| ||||||
Ngazi za chini | ||||||
|
Sifongo-bahari ni wanyama sahili wa maji (bahari na baridi) katika faila Porifera (maana: walio na vinyweleo) ambao wamekazika chini, ijapokuwa spishi chache zinaweza kwenda kwa mbio wa mm 1-4 kwa siku. Spishi nyingi sana zina umbo wa yai, bonge au bomba. Kuna kipenyo kikubwa kiasi juu yao (osculum au kidomo) na vinyweleo vidogo vingi (ostia) kila sehemu ya mwili.
Mwili wa sifongo ni ukuta wa seli tu ambao unazunguka uwazi wa katikati. Ukuta huu umeumbwa kwa tabaka la kolajini (collagen) au mesohili (mesohyl) lililofunikwa na seli nje na ndani. Hata vinyweleo vimezungukwa na seli zinazoitwa porositi (porocytes). Seli zenye kijeledi (flagellum), ambazo huitwa koanositi (choanocytes), zisukuma maji kuelekea osculum na maji mengine yaingia kupitia ostia. Chembe za kulika zilizomo majini ziliwa kwa phagocytosis.
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Sifongo-bahari, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.