Polokwane (kwa Kiafrikaans: Pietersburg) ni manisipaa ya Afrika Kusini na mji mkuu wa Jimbo la Limpopo.
Jiji la Polokwane | |
Mahali pa mji wa Polokwane katika Afrika Kusini | |
Majiranukta: 23°53′24″S 29°27′0″E / 23.89000°S 29.45000°E | |
Nchi | Afrika Kusini |
---|---|
Majimbo | Limpopo |
Idadi ya wakazi | |
- Wakazi kwa ujumla | 123,749 |
Tovuti: www.polokwane.org.za |
Mji ulianzishwa mwaka 1886 na makaburu wa Voortrekker ukapewa jina la Pietersburgh kwa heshima ya jenerali ya makaburu Petrus Jacobus "Piet" Joubert. Wakati wa Vita ya pili ya Waingereza dhidi ya Makaburu Pietersburgh ikawa mji mkuu wa jamhuri ya Transvaal ikavamiwa na Waingereza mwaka 1901.
Polokwane iko katika nyanda za juu kwa kimo cha mita 1,312. Hali ya hewa ni ya wastani yenye sentigredi 27°C wakati wa joto na 20°C wakati wa baridi.
Kuna migodi ya almasi na kiwanda cha kuchimbia mchanga safi sana unaofaa matumizi ya vioo. Pamoja na migodi kuna pia viwanda mbalimbali.
Polokwane iliona michezo ya mpira wakati wa kombe la dunia la 2010. Polokwane pia ni jina la timu ya mpira wa miguu, na ndiyo makao makuu ya timu hiyo ijulikanayo kama "Polokwane Football Club"
Makala hii kuhusu maeneo ya Afrika Kusini bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Polokwane kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Polokwane, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.