Gadolini (Gadolinium) ni elementi ya kikemia yenye alama Gd na namba atomia 64.
Gadolini ni metali yenye rangi nyeupe-ya kifedha wakati haijaoksidika bado. Gadolini humenyuka na oksijeni ya hewani au unyevu polepole ikiunda mpako mweusi. Chini ya °C 20 ina tabia za kisumaku.
Kiasili hupatikana hasa kwa umbo la oksidi.
Jina lake limetokana na madini ya gadoliniti inamopatikana; madini yalipewa jina kwa heshima ya moja ya madini ambayo gadolinium hupatikana, yenye jina kwa mwanakemia Johan Gadolin kutoka Uswidi.
Gadolinium ina tabia kadhaa zisizo kawaida. Katika kampaundi za feleji nyongeza ndogo ya Gadolini hupunguza hupunguza utendanaji wake na oksijeni katika hali ya joto.[ onesha inahitajika ]
Kampaundi za gadolini hutumiwa katika mikrowevu, uzalishaji wa diski za kompyuta na pia kwa skrini za rada.
Upatikanaji katika ganda la Dunia ni takribani miligramu 6.2 kwa kila kilogramu. Huchimbwa hasa China, Marekani, Brazil, Sri Lanka, Uhindi na Australia. Uzalishaji wa gadolini safi duniani ni karibu tani 400 kwa mwaka.
Makala hii kuhusu mambo ya kemia bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Gadolini kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Gadolini, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.