Tenno ni cheo cha mfalme au kaisari wa Japani.
Kufuatana na katiba ya nchi yeye ni "ishara wa dola na wa umoja wa taifa".
Tenno wa sasa ni Naruhito (tangu mwaka 2019, alipomrithi baba yake).
Historia ya Japani inamkumbuka tenno wa kwanza kabisa aliyekuwa Jimmu mnamo 660 KK. Wataalamu wengine huwa na shaka lakini wanakubali ya kwamba watawala hao walikuwepo angalau tangu karne ya 5 BK. Hadi karne ya 19 ikulu yao ilikuwa mjini Kyoto, lakini tangu Meiji iko Tokyo.
Nasaba ya watawala wa Japani ni nasaba ya kale zaidi duniani.
Katika historia hiyo ndefu matenno walikuwa na madaraka tofautitofauti. Hata kama walitazamwa kama wakuu wa taifa hali halisi madaraka yao yalikuwa madogo wakati mwingine. Lakini kulikuwa pia na matenno walioamua kabisa juu ya siasa ya nchi kwa mfano Meiji tangu mwaka 1868.
Makala hii kuhusu mambo ya siasa bado ni mbegu. Unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuongezea habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Tenno, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.