Soweto ni sehemu ya jiji la Johannesburg, Afrika Kusini.
Jina hilo ni kifupi cha Southwestern townships yaani "mapambizo ya kusini-magharibi". Hayo yalianzishwa wakati wa apartheid kama makazi ya Waafrika pekee, na kwa hiyo yalitazamwa kuwa "mapambizo meusi" ya Johannesburg.
Kati ya miaka 1983 na 2002 Soweto ilikuwa manisipaa ya pekee, baadaye imekuwa tena sehemu ya jiji la Johannesburg.
Wakati wa sensa ya mwaka 2008 idadi ya wakazi ilikuwa milioni 1.3 na hii inalingana na theluthi moja ya wakazi wote wa jiji hilo.
Ndani ya Soweto kuna vitongoji mbalimbali, idadi inatajwa mara kuwa 29, mara 34. Kati yake, vingine ni maeneo maskini sana, hata mitaa ya vibanda; vingine vina nyumba nzuri.
Soweto ilikuwa kitovu cha upinzani wa wanafunzi dhidi ya apartheid kwenye mwaka 1976.
|url-access=
ignored (help)Makala hii kuhusu maeneo ya Afrika Kusini bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Soweto kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Soweto, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.