Shirika la Kenya la Wanyama Pori (KWS - Kenya Wildlife Service) lilianzishwa mwaka 1990.
Inasimamia uasilia na viumbe hai wa nchi, ikilinda na kuhifadhi flora na fauna.
KWS inasimamia mbuga za wanyama za kitaifa na hifadhi nchini Kenya. Fedha zinazokusanywa kama ada ya kiingilio hutumika kusaidia uhifadhi wa mimea na wanyama ndani ya hifadhi au mbuga.
Kenya ina mbuga na hifadhi 35 teule za kitaifa:
KWS inaendesha mipango maalum kusaidia viumbe na makazi ya Kenya ambayo yako kwenye hatari hasa. Wana mipango ya uhifadhi wa sehemu za chemchemi na misitu,na miradi maalum ya tembo na kifaru kusaidia kuwaokoa kutoka kwa wawindaji. Hirola, ambayo iko katika hatari ya kupotea, pia inafuatiliwa.
Ndani ya KWS kuna huduma kadhaa, kila moja ikiwajibika kwa eneo tofauti la kazi:
Hili tawi la KWS hufanya kazi nje ya hifadhi za taifa. Wao badala hufanya kazi katika maeneo kama vile kanda za wanyamapori, na kufundisha jamii wanaoishi huko kuhamasisha uhifadhi na kuchunga rasilimali zao.
Kazi ya huduma hii ni kuondoa uwindaji katika hifadhi za kitaifa, na kukomesha biashara haramu.
Huduma hii huhakikisha kuwa afya ya kuzaliana ya wakazi wa aina inazingatiwa kote nchini.
KWS ina kituo cha mafunzo mjini Naivasha. Watumishi wa KWS hufundishwa hapa, na pia mafunzo kwa wanafunzi wa nje wa ikolojia na utalii.
KWS inendesha vituo kadhaa vya elimu:
Hizi ziko ndani ya Hifadhi za Taifa, na huendesha mipango ya kuhamasisha watu kuhudumia na kulinda mazingira yao. Imelengwa kwa wananchi, hasa makundi ya shule, lakini ni wazi kwa mtu yeyote.
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Shirika la Huduma kwa Wanyama Pori ya Kenya, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.