Papa (neno la mkopo kutoka Kilatini lakini lenye asili ya Kigiriki, πάππας, pappas, jina ambalo mtoto anamuitia baba yake)ni cheo cha kiongozi mkuu wa Kanisa Katoliki duniani kote.
Cheo hicho kinategemea kile cha askofu wa Roma.
Hii ni sehemu ya mfululizo kuhusu Kanisa Katoliki | |
Imani | |
---|---|
Umoja wa Mungu | |
Muundo | |
Papa: Fransisko | |
Historia | |
Historia Ukristo | |
Ibada | |
Liturujia Mwaka wa Kanisa | |
Mapokeo ya liturujia | |
Liturujia ya Kilatini (Roma Liturujia ya Trento Milano Toledo Braga Lyon Canterbury) |
Kiasili neno la Kilatini "Papa" linamaanisha "Baba", nalo likawa cheo kutokana na nia ya kumtaja askofu wa Roma kwa heshima ya pekee. Msingi wa heshima hiyo ni imani ya Wakatoliki kuwa askofu wa Roma ni mwandamizi wa Petro, mkuu wa mitume wa Yesu.
Wakatoliki huamini ya kwamba Petro alipewa na Yesu kazi ya kuongoza Kanisa lote kwa niaba yake na ya kwamba jukumu hilo linaendelea kati ya waandamizi wa Petro kwenye kiti cha askofu wa Roma ambacho kwa heshima kinaitwa Ukulu mtakatifu.
Upapa ni kati ya vyeo vya zamani zaidi duniani na umeathiri sana historia ya binadamu kwa miaka karibu 2000.Athari hiyo iliweza kuwa nzuri au mbaya, kadiri ya matendo ya mhusika.
Kwa muda mrefu mamlaka ya Papa upande wa siasa, hasa juu ya mikoa ya Italia ya Kati, ilisababisha nchi nyingine na koo tajiri za Roma zijiingize katika uchaguzi ili kupitisha watu wao, hata wasiofaa. Upande mwingine, Mapapa waliathiriwa na utamaduni na mazingira ya nyakati zao, hasa tapo la Renaissance, kiasi cha kuzama katika anasa.
Baada ya Dola la Papa kutekwa na Ufalme wa Italia (1860-1870), Mapapa wameweza kushughulikia zaidi mambo ya kiroho na kujitokeza kwa ubora.Kwa miaka ya karibuni inatosha kumfikiria Papa Yohane Paulo II na mchango wake katika kuangusha ukomunisti katika Ulaya Mashariki.
Papa huchaguliwa na makardinali wa Kanisa Katoliki baada ya mtangulizi wake kufa au kung'atuka. Baada ya kuchaguliwa papa mpya anaweza akajipatia jina jipya. Tangu tarehe 13 Machi 2013 ni Papa Fransisko, ambaye awali aliitwa Jorge Mario Bergoglio, kutoka Argentina.
Majina ya mapapa wengine wa Kanisa Katoliki yanapatikana katika orodha ya mapapa.
Papa ni pia mkuu wa nchi huru ya Mji wa Vatikano iliyopo ndani ya mji wa Roma (ambao ni mji mkuu wa Italia).
Cheo cha Papa hutumiwa pia na baadhi ya madhehebu mengine ya Kikristo kwa viongozi wao, hasa kwa mkuu wa Kanisa la Kikopti huko Misri.
Makala hii kuhusu Kanisa Katoliki bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Papa kama historia yake au maelezo zaidi? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Papa, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.