Ukatili (kutoka neno la Kiarabu) ni hali ya kusababisha kwa makusudi mateso na kukosesha raha dhidi ya mtu mwingine, ilihali suluhisho la wazi linapatikana kwa urahisi.
Ukatili unaweza kutokana na matatizo ya kisaikolojia yenye mizizi utotoni, lakini pia ni tabia ambayo mtu anaweza kujijengea kinyume cha maadili.
Ukatili unaweza kujitokeza hata katika namna ya kufanya ngono.
Neno ukatili mara nyingi hutumika katika sheria kuhusu matendo dhidi ya watoto, wenzi wa ndoa, na wafungwa lakini pia dhidi ya wanyama. Ukatili kwa wanyama unapojadiliwa, mara nyingi humaanisha mateso yasiyofaa, yaani yasiyo na sababu ya kutosha, si yale yanayotakiwa na ulaji wa nyama yake.
Katika sheria ya jinai, inamaanisha mateso, unyanyasaji na adhabu kali na isiyo ya kawaida. Katika visa vya talaka, mamlaka nyingi huiruhusu kwa ajili ya matendo ya kikatili na ya kinyama. Katika sheria, ukatili ni "usumbufu wa kimwili au kiakili, haswa inapofikiriwa kwa uamuzi wa kutoa talaka."
Makala bado ni mbegu. Unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuongezea habari. |
This article uses material from the Wikipedia Kiswahili article Ukatili, which is released under the Creative Commons Attribution-ShareAlike 3.0 license ("CC BY-SA 3.0"); additional terms may apply (view authors). Maudhui yanapatikana kwa chini ya CC BY-SA 4.0 isipokuwa iwe imebainishwa vinginevyo. Images, videos and audio are available under their respective licenses.
®Wikipedia is a registered trademark of the Wiki Foundation, Inc. Wiki Kiswahili (DUHOCTRUNGQUOC.VN) is an independent company and has no affiliation with Wiki Foundation.